395 – ´Uqbah bin ´Aamir (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Tulikuwa pamoja na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Tulikuwa tunamuhudumia wenyewe na tunawachunga ngamia wetu kwa kupokezana. Wakati ilipokuwa zamu yangu, basi nikawatoa wakati wa asubuhi ambapo nikamuona Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesimama akisema:
ما مِنكم مِن أحدِ يتوّضأُ فيُحسِنُ الوضوءَ، ثمّ يقوم فيركع ركعتين يُقبلُ عليهما بقلبِه ووجهه؛ إلا قد أوجَبَ . فقلتُ: بخٍ بخٍ! ما أجودَ هذه
“Hakuna yeyote katika nyinyi atakayetawadha akatia vizuri wudhuu´ wake kisha akasimama na kuswali Rak´ah mbili, akaziuelekezea moyo wake na uso wake, isipokuwa itamthubutukia.” Ndipo nikasema: “Bishara, bishara! Ni ukarimu uliyoje huu!”[1]
Ameipokea Muslim, Abu Daawuud, na tamko ni lake, an-Nasaa’iy, Ibn Maajah, Ibn Khuzaymah na al-Haakim, isipokuwa kwake imekuja:
ما مِن مسلم يتوضأ فيُسبغُ الوضوءَ ثم يقوم في صلاته، فيعلمُ ما يقول؛ إلاَّ انفتل وهو كيومَ ولدته أُمه
“Hakuna muislamu yeyote atakayetawadha na akaeneza vizuri wudhuu´ kisha akasimama katika swalah yake na huku akieleza kile anachokisema, isipokuwa ataimaliza akiwa msafi kama ile siku aliyozaliwa na mama yake.”[2]
Halafu akasema:
“Cheni yake ya wapokezi ni Swahiyh.”
Kumthubutukia maana yake ni kwamba amefanya yale yanayomthubutukia yeye kuingia Peponi.”
[1] Swahiyh.
[2] Swahiyh.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/282-283)
- Imechapishwa: 30/01/2024
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
395 – ´Uqbah bin ´Aamir (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Tulikuwa pamoja na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Tulikuwa tunamuhudumia wenyewe na tunawachunga ngamia wetu kwa kupokezana. Wakati ilipokuwa zamu yangu, basi nikawatoa wakati wa asubuhi ambapo nikamuona Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesimama akisema:
ما مِنكم مِن أحدِ يتوّضأُ فيُحسِنُ الوضوءَ، ثمّ يقوم فيركع ركعتين يُقبلُ عليهما بقلبِه ووجهه؛ إلا قد أوجَبَ . فقلتُ: بخٍ بخٍ! ما أجودَ هذه
“Hakuna yeyote katika nyinyi atakayetawadha akatia vizuri wudhuu´ wake kisha akasimama na kuswali Rak´ah mbili, akaziuelekezea moyo wake na uso wake, isipokuwa itamthubutukia.” Ndipo nikasema: “Bishara, bishara! Ni ukarimu uliyoje huu!”[1]
Ameipokea Muslim, Abu Daawuud, na tamko ni lake, an-Nasaa’iy, Ibn Maajah, Ibn Khuzaymah na al-Haakim, isipokuwa kwake imekuja:
ما مِن مسلم يتوضأ فيُسبغُ الوضوءَ ثم يقوم في صلاته، فيعلمُ ما يقول؛ إلاَّ انفتل وهو كيومَ ولدته أُمه
“Hakuna muislamu yeyote atakayetawadha na akaeneza vizuri wudhuu´ kisha akasimama katika swalah yake na huku akieleza kile anachokisema, isipokuwa ataimaliza akiwa msafi kama ile siku aliyozaliwa na mama yake.”[2]
Halafu akasema:
“Cheni yake ya wapokezi ni Swahiyh.”
Kumthubutukia maana yake ni kwamba amefanya yale yanayomthubutukia yeye kuingia Peponi.”
[1] Swahiyh.
[2] Swahiyh.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/282-283)
Imechapishwa: 30/01/2024
Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
https://firqatunnajia.com/13-hadiyth-hakuna-yeyote-katika-nyinyi-atakayetawadha/