Swali 12: Nimewasikia wengi wasiokuwa na elimu wakisema kwamba mke anaharamika kwa mume wake baada ya kufa kwake na kwamba haijuzu kumwangalia wala kumweka kwenye mwanandani kaburi lake. Je, haya ni sahihi[1]?
Jibu: Dalili za ki-Shari´ah zimejulisha ya kwamba hapana vibaya kwa mke kumuosha mume wake na kumwangalia. Aidha hapana vibaya kwake mume kumuosha na kumwangalia. Asmaa´ bint ´Umays (Radhiya Allaahu ´anhaa) alimuosha mume wake Abu Bakr as-Swiddiyq (Radhiya Allaahu ´anh). Vilevile Faatwimah aliacha anausia ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ndiye amuoshe.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (13/109-110).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 18
- Imechapishwa: 12/12/2021
Swali 12: Nimewasikia wengi wasiokuwa na elimu wakisema kwamba mke anaharamika kwa mume wake baada ya kufa kwake na kwamba haijuzu kumwangalia wala kumweka kwenye mwanandani kaburi lake. Je, haya ni sahihi[1]?
Jibu: Dalili za ki-Shari´ah zimejulisha ya kwamba hapana vibaya kwa mke kumuosha mume wake na kumwangalia. Aidha hapana vibaya kwake mume kumuosha na kumwangalia. Asmaa´ bint ´Umays (Radhiya Allaahu ´anhaa) alimuosha mume wake Abu Bakr as-Swiddiyq (Radhiya Allaahu ´anh). Vilevile Faatwimah aliacha anausia ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ndiye amuoshe.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (13/109-110).
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 18
Imechapishwa: 12/12/2021
https://firqatunnajia.com/12-mafungamano-ya-kindoa-hayamalizika-kwa-kifo/