55 – Abu Mu´aawiyah ametuhadithia, kutoka kwa al-A´mash, kutoka kwa Abu Sufyaan, kutoka kwa Anas aliyesimulia:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akikithirisha kusema:
يا مقلب القلوب ثبت قلبي على دينك
“Ee mwenye kuzigeuza nyoyo! Uthibitishe moyo wangu juu ya dini Yako.”
Wakasema: “Ee Mtume wa Allaah! Tumekuamini, na yale uliyokuja nayo; je, unachelea kwetu?” Akasema: “Ndio. Hakika nyoyo ziko kati ya vidole viwili katika vidole vya Mwingi wa huruma (´Azza wa Jall). Anazigeuza.”[1]
56 – Mu´aadh bin Mu´aadh ametuhadithia: Abu Ka´b mzee wa hariri ametueleza: Shihr bin Hawshab ametueleza:
“Nilisema kumwambia Umm Salamah: “Ee mama wa waumini, ni ipi du´aa aliyokuwa akiomba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anapokuwa kwako?” Akasema: “Du´aa yake nyingi ilikuwa:
يا مقلب القلوب ثبت قلبي على دينك
“Ee mwenye kuzigeuza nyoyo! Uthibitishe moyo wangu juu ya dini Yako.”
Akasema: “Ee Umm Salamah! Hakuna mwanadamu yeyote isipokuwa moyo wake uko kati ya vidole viwili katika vidole vya Mwingi wa huruma. Akitaka anaunyoosha, na akitaka anaupindisha.”
57 – Yaziyd bin Haaruun ametuhadithia: Hammaam bin Yahyaa ametueleza, kutoka kwa ´Aliy bin Zayd, kutoka kwa Umm Muhammad, kutoka kwa ´Aaishah ambaye amesema:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisema:
يا مقلب القلوب ثبت قلبي على دينك
“Ee mwenye kuzigeuza nyoyo! Uthibitishe moyo wangu juu ya dini Yako.”
Nikasema: “Ee Mtume wa Allaah, hakika wewe unaomba du´aa hii?” Akasema: “Ee ´Aaishah, hujui kuwa moyo wa mwanadamu uko kati ya vidole viwili vya Allaah? Akitaka kuipindua katika uongofu, basi anaipindua, na akitaka kuipindua katika upotofu, basi anaipindua.”
[1] at-Tirmidhiy (3522) na Ibn Maajah (3834) Cheni ya wapokezi ni Swahiyh kwa mujibu wa sharti za Muslim. Ahmad (3/257) ameipokea kupitia njia nyingine kutoka kwa al-A´mash, na at-Tirmidhiy, kupitia kwa Abu Mu´aawiyah, ambaye amesema kuwa Hadiyth ni nzuri. Amezidisha katika nyingine ”Anaupindisha anavyotaka.”
- Mhusika: Imaam Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin Abiy Shaybah al-Kuufiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kitaab-ul-Iymaan, uk. 28
- Imechapishwa: 10/07/2023
- taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)