Miongoni mwa kuwakata Ahl-ul-Bid´ah ni kuacha kuangalia na kusoma vitabu vyao kwa kuchelea fitina au kuvisambaza kati ya watu. Kujitenga na yale maeneo ya upotofu ni jambo la lazima. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhusu ad-Dajjaal:
“Atakayesikia juu yake basi ajitenge naye. Naapa kwa Allaah mtu atamwendea na yeye anajiona kuwa ni muumini hatimaye amfuate kutokana na zile shubuha atazomuweka nazo.”
Ameipokea Abu Daawuud. al-Albaaniy amesema:
“Cheni ya wapokezi wake ni Swahiyh.”[1]
Lakini ikiwa malengo ya kuangalia na kusoma vitabu vyao ni kutaka kuzijua zile Bid´ah zao ili aziraddi hapana vibaya kwa yule ambaye yuko na ´Aqiydah sahihi itayoweza kumlinda na vilevile akawa na uwezo wa kuwaraddi. Pengine kufanya hivo ikawa ni jambo la lazima. Kwa sababu ni lazima kuzirudisha nyuma Bid´ah. Jambo ambalo la lazima halitimii isipokuwa kwa jambo hilo basi nalo litakuwa ni lazima.
[1] Ahmad (04/43, 441), Abu Daawuud (4319) na al-Haakim (04/531). Ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh-ul-Jaamiy´” (6301) nna katika “Takhriyj-ul-Mishkaah” (5488).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ta´aliyq mukhtaswar ´alaa Lum´at-il-I´tiqaad, uk. 159-160
- Imechapishwa: 20/02/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)