07 – Mke kumuomba na kumg´ang´ania mume amwache
Anamuomba mume wake talaka wakati anapoingia na wakati anapotoka. Masikini huyu hajui kuwa ameingia katika dhambi kubwa asipokuwa na sababu inayokubalika kwa mujibu wa Shari´ah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ametahadharisha jambo hilo na akawatishia Maswahabah zake. Thawbaan (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Mwanamke yeyote ambaye anamuomba mume wake talaka pasi na sababu, basi ni haramu kwake harufu ya Pepo.”[1]
Ameipokea Ibn Maajah na ni Hadiyth Swahiyh.
Vilevile Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Mwanamke hamuombi mume wake talaka pasi na neno ambapo akapata harufu ya Pepo. Hakika Pepo yake inapatikana mwendo wa miaka arobaini.”[2]
Ameipokea Ibn Maajah (2054).
Kwa hivyo mwanamke anayemuomba mume wake talaka yuko katika khatari kubwa.
[1] Ibn Maajah (2055). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”al-Irwaa´” (2036).
[2] Ibn Maajah (2054). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Dhwa´iyf Ibn Maajah” (445).
- Muhusika: Shaykh Jamaal bin Furahyaan al-Haarithiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Twalaaq – asbaabuhu wa ´ilaajuh, uk. 26-27
- Imechapishwa: 04/04/2024
07 – Mke kumuomba na kumg´ang´ania mume amwache
Anamuomba mume wake talaka wakati anapoingia na wakati anapotoka. Masikini huyu hajui kuwa ameingia katika dhambi kubwa asipokuwa na sababu inayokubalika kwa mujibu wa Shari´ah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ametahadharisha jambo hilo na akawatishia Maswahabah zake. Thawbaan (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Mwanamke yeyote ambaye anamuomba mume wake talaka pasi na sababu, basi ni haramu kwake harufu ya Pepo.”[1]
Ameipokea Ibn Maajah na ni Hadiyth Swahiyh.
Vilevile Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Mwanamke hamuombi mume wake talaka pasi na neno ambapo akapata harufu ya Pepo. Hakika Pepo yake inapatikana mwendo wa miaka arobaini.”[2]
Ameipokea Ibn Maajah (2054).
Kwa hivyo mwanamke anayemuomba mume wake talaka yuko katika khatari kubwa.
[1] Ibn Maajah (2055). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”al-Irwaa´” (2036).
[2] Ibn Maajah (2054). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Dhwa´iyf Ibn Maajah” (445).
Muhusika: Shaykh Jamaal bin Furahyaan al-Haarithiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Twalaaq – asbaabuhu wa ´ilaajuh, uk. 26-27
Imechapishwa: 04/04/2024
https://firqatunnajia.com/11-sababu-ya-saba-ya-talaka-ambayo-ni-kungangania-mume-ampe-talaka/