Ni vipi yanafikiwa mapenzi na ulinzi (الولاية) wa Allaah? Yanafikiwa kwa sifa mbili ambazo Allaah amezibainisha ndani ya Kitabu Chake. Allaah (Ta´ala) amesema:
أَلَا إِنَّ أَوْلِيَاءَ اللَّـهِ لَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ الَّذِينَ آمَنُوا وَكَانُوا يَتَّقُونَ
“Tanabahi! Hakika mawalii wa Allaah hawana khofu juu yao na wala hawatohuzunika. Ambao wameamini na wakawa wanamcha.”[1]
Sifa moja inahusiana na moyo na nyingine inahusiana na viungo vya mwili.
الَّذِينَ آمَنُوا
”Ambao wameamini… ”
Ni moyoni.
وَكَانُوا يَتَّقُونَ
”… na wakawa wanamcha.”[2]
Hii ni katika viungo vya mwili.
Wakati moyo na viungo vya mwili vinapotengemaa, basi mtu anapata mapenzi na ulinzi kwa sifa hizi mbili. Mawalii sio wale wanaojidai ambao wanafuata njia za watawa na Ahl-ul-Bid´ah ambao wanazusha ndani ya Shari´ah ya Allaah yale yasiyokuwemo na kujidai eti wao ndio mawalii. Kwa hivyo mapenzi ya Allaah (´Azza wa Jall) ambayo ndio yanamtukuza mtu yanapatikana kwa sifa hizi mbili:
1 – Imani.
2 – Kumcha Allaah.
[1] 10:62-63
[2] 10:62-63
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Du´aa´ al-Qunuut-il-Witr, uk. 16-17
- Imechapishwa: 10/03/2024
Ni vipi yanafikiwa mapenzi na ulinzi (الولاية) wa Allaah? Yanafikiwa kwa sifa mbili ambazo Allaah amezibainisha ndani ya Kitabu Chake. Allaah (Ta´ala) amesema:
أَلَا إِنَّ أَوْلِيَاءَ اللَّـهِ لَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ الَّذِينَ آمَنُوا وَكَانُوا يَتَّقُونَ
“Tanabahi! Hakika mawalii wa Allaah hawana khofu juu yao na wala hawatohuzunika. Ambao wameamini na wakawa wanamcha.”[1]
Sifa moja inahusiana na moyo na nyingine inahusiana na viungo vya mwili.
الَّذِينَ آمَنُوا
”Ambao wameamini… ”
Ni moyoni.
وَكَانُوا يَتَّقُونَ
”… na wakawa wanamcha.”[2]
Hii ni katika viungo vya mwili.
Wakati moyo na viungo vya mwili vinapotengemaa, basi mtu anapata mapenzi na ulinzi kwa sifa hizi mbili. Mawalii sio wale wanaojidai ambao wanafuata njia za watawa na Ahl-ul-Bid´ah ambao wanazusha ndani ya Shari´ah ya Allaah yale yasiyokuwemo na kujidai eti wao ndio mawalii. Kwa hivyo mapenzi ya Allaah (´Azza wa Jall) ambayo ndio yanamtukuza mtu yanapatikana kwa sifa hizi mbili:
1 – Imani.
2 – Kumcha Allaah.
[1] 10:62-63
[2] 10:62-63
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Du´aa´ al-Qunuut-il-Witr, uk. 16-17
Imechapishwa: 10/03/2024
https://firqatunnajia.com/11-ni-vipi-nitakuwa-mpenzi-na-walii-wa-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)