Swali 11: Ni ipi hukumu ya swawm iliyopendekezwa kama mfano wa zile siku sita za Shawwaal, zile siku kumi za Dhul-Hijjah na siku ya ´Aashuuraa´ kwa yule ambaye anadaiwa baadhi ya siku za Ramadhaan?
Jibu: Kwa yule ambaye analazimika kulipa deni lake la Ramadhaan ni lazima kwake aanze kulilipa kabla ya swawm ya Sunnah. Kwa sababu faradhi ni muhimu zaidi kuliko ´ibaadah iliyopendekezwa. Haya ndio maoni yenye nguvu zaidi ya wanachuoni.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdllaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: As-ilah Muhimmah tata´alaqah bisw-Swiyaam, uk. 19
- Imechapishwa: 20/04/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)