Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Kwamba mimi nadai Ijtihaad na kwamba mimi nimetoka nje ya Taqliyd.
MAELEZO
Kwamba mimi nadai Ijtihaad – Wanasema juu yake kwamba anadai kwamba ni mwenye kujitegemea katika Ijtihaad na kwamba anakinzana na wale maimamu wanne. Huu ni uongo. Shaykh ni Hanbaliy. Lakini hata hivo hafanyii ushabiki madhehebu ya imamu wake. Anafuata yale ambayo dalili zake ni zenye nguvu ijapokuwa ni kutoka kwa imamu mwingine. Kwa sababu ni mwenye kutaka haki. Ni kama mfano wa Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah, Ibn-ul-Qayyim na wengineo katika wahakiki. Hawafanyi ushabiki. Wanatendea kazi yale yaliyosimama juu ya dalili. Lakini hawatoki nje ya madhehebu manne ambayo ndio madhehebu ya maimamu ambayo wamesoma, wakayajua, kuyahariri na wakayarithi waislamu kizazi kwa kizazi. Kwa hiyo hadai Ijtihaad isiyofungamanishwa. Kwa msemo mwingine ni kwamba hadai kuwa yuko katika safu za wale maimamu wanne; kama Abu Haniyfah, Maalik, ash-Shaafi´iy, Ahmad na al-Awzaa´iy. Lakini wanamsemea uongo. Maneno yake:
“… kwamba mimi nimetoka nje ya Taqliyd.”
Ni kule kukubali maoni ya mwanachuoni bila ya kutambua dalili yake. Taqliyd imegawanyika mafungu mawili:
La kwanza: Kufuata kipofu ambapo mtu akafanyia ushabiki maoni ya mwanachuoni fulani ijapokuwa ni yenye kwenda kinyume na dalili. Shaykh Muhammad na wengineo hawanfanyi hivo.
La pili: Kufuata kwa haki. Ni kama mfano wa kuchukua maoni ya mwanachuoni pale yanapoafikiana na dalili. Huku ni kufuata kwa haki. Huku ni kuwafuata watu wa haki. Kunaitwa pia Taqliyd au kufuata. Maana yake ni moja. Yuusuf (´alayhis-Salaam) alisema:
وَاتَّبَعْتُ مِلَّةَ آبَائِي إِبْرَاهِيمَ وَإِسْحَاقَ وَيَعْقُوبَ
“Nimefuata mila ya baba zangu; Ibraahiym na Ishaaq na Ya’quub.”[1]
Huku ni kufuata kwa haki.
وَالسَّابِقُونَ الْأَوَّلُونَ مِنَ الْمُهَاجِرِينَ وَالْأَنصَارِ وَالَّذِينَ اتَّبَعُوهُم بِإِحْسَانٍ
“Na wale waliotangulia wa mwanzo miongoni mwa Muhaajiruun na Answaar na wale waliowafuata kwa wema… ”[2]
Huku wanaita ni kufuata. Yule aliye juu ya haki basi sisi tunamfuata.
[1] 12:38
[2] 09:100
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Aqiydat-il-Imaam Mujaddid Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab, uk. 146
- Imechapishwa: 07/06/2021
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Kwamba mimi nadai Ijtihaad na kwamba mimi nimetoka nje ya Taqliyd.
MAELEZO
Kwamba mimi nadai Ijtihaad – Wanasema juu yake kwamba anadai kwamba ni mwenye kujitegemea katika Ijtihaad na kwamba anakinzana na wale maimamu wanne. Huu ni uongo. Shaykh ni Hanbaliy. Lakini hata hivo hafanyii ushabiki madhehebu ya imamu wake. Anafuata yale ambayo dalili zake ni zenye nguvu ijapokuwa ni kutoka kwa imamu mwingine. Kwa sababu ni mwenye kutaka haki. Ni kama mfano wa Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah, Ibn-ul-Qayyim na wengineo katika wahakiki. Hawafanyi ushabiki. Wanatendea kazi yale yaliyosimama juu ya dalili. Lakini hawatoki nje ya madhehebu manne ambayo ndio madhehebu ya maimamu ambayo wamesoma, wakayajua, kuyahariri na wakayarithi waislamu kizazi kwa kizazi. Kwa hiyo hadai Ijtihaad isiyofungamanishwa. Kwa msemo mwingine ni kwamba hadai kuwa yuko katika safu za wale maimamu wanne; kama Abu Haniyfah, Maalik, ash-Shaafi´iy, Ahmad na al-Awzaa´iy. Lakini wanamsemea uongo. Maneno yake:
“… kwamba mimi nimetoka nje ya Taqliyd.”
Ni kule kukubali maoni ya mwanachuoni bila ya kutambua dalili yake. Taqliyd imegawanyika mafungu mawili:
La kwanza: Kufuata kipofu ambapo mtu akafanyia ushabiki maoni ya mwanachuoni fulani ijapokuwa ni yenye kwenda kinyume na dalili. Shaykh Muhammad na wengineo hawanfanyi hivo.
La pili: Kufuata kwa haki. Ni kama mfano wa kuchukua maoni ya mwanachuoni pale yanapoafikiana na dalili. Huku ni kufuata kwa haki. Huku ni kuwafuata watu wa haki. Kunaitwa pia Taqliyd au kufuata. Maana yake ni moja. Yuusuf (´alayhis-Salaam) alisema:
وَاتَّبَعْتُ مِلَّةَ آبَائِي إِبْرَاهِيمَ وَإِسْحَاقَ وَيَعْقُوبَ
“Nimefuata mila ya baba zangu; Ibraahiym na Ishaaq na Ya’quub.”[1]
Huku ni kufuata kwa haki.
وَالسَّابِقُونَ الْأَوَّلُونَ مِنَ الْمُهَاجِرِينَ وَالْأَنصَارِ وَالَّذِينَ اتَّبَعُوهُم بِإِحْسَانٍ
“Na wale waliotangulia wa mwanzo miongoni mwa Muhaajiruun na Answaar na wale waliowafuata kwa wema… ”[2]
Huku wanaita ni kufuata. Yule aliye juu ya haki basi sisi tunamfuata.
[1] 12:38
[2] 09:100
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh ´Aqiydat-il-Imaam Mujaddid Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab, uk. 146
Imechapishwa: 07/06/2021
https://firqatunnajia.com/106-radd-juu-ya-uongo-wa-ibn-suwhaym-kwamba-shaykh-anadai-ijtihaad/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)