Malaika wengine wamepewa kazi ya kumlinda mwanadamu asifikwe na majanga na kushambuliwa. Allaah (Ta´ala) amesema:
لَهُ مُعَقِّبَاتٌ مِّن بَيْنِ يَدَيْهِ وَمِنْ خَلْفِهِ يَحْفَظُونَهُ مِنْ أَمْرِ اللَّـهِ
“Ana Malaika wanaofuatana kwa zamu mbele yake na nyuma yake wanamhifadhi kwa amri ya Allaah.”[1]
Wanamuhifadhi mtu kwa amri ya Allaah mpaka pale yatapomfika makadirio ya Allaah; basi kipindi hicho wanamwacha na matokeo yake anafikwa na yale aliyompangia Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Kwa ajili hiyo mtu anaweza kufikwa na hali ya khatari kabisa lakini hata hivyo akasalimika, kwa sababu yuko pamoja naye Malaika wanaomuhifadhi kutokana na amri ya Allaah (´Azza wa Jall). Hawa ndio Malaika wanaofuatana.
[1] 13:11
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bayaan-ul-Ma´aaniy fiy Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy, uk. 80
- Imechapishwa: 31/08/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)