Huyu hapa Nabii wa mwisho kiongozi wao na bwana wa wanadamu Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Allaah amesema juu yao:
وَإِذْ يَمْكُرُ بِكَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِيُثْبِتُوكَ أَوْ يَقْتُلُوكَ أَوْ يُخْرِجُوكَ ۚ وَيَمْكُرُونَ وَيَمْكُرُ اللَّـهُ ۖ وَاللَّـهُ خَيْرُ الْمَاكِرِينَ
“Pindi walipokupangia vitimbi wale waliokufuru ili wakufunge, au wakuue, au wakutoe [nje ya Makkah]. Na wanapanga vitimbi na Allaah anapanga vitimbi; na Allaah ni mbora wa wenye kupanga vitimbi.”[1]
وَقَالُوا يَا أَيُّهَا الَّذِي نُزِّلَ عَلَيْهِ الذِّكْرُ إِنَّكَ لَمَجْنُونٌ
”Wakasema: ”Ee ambaye umeteremshiwa Ukumbusho, hakika wewe bila shaka ni mwendawazimu.”[2]
يَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُو آلِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍ
”Wanasema: ”Je, sisi kweli tuache waabudiwa wetu kwa ajili ya mshairi mwendawazimu?”[3]
Alifikwa na maudhi ya kimaneno na ya kimatendo ambayo yanatambulika kwa wanazuoni katika historia. Pamoja na hivyo akasubiri na mwisho mwema ukawa wake.
[1] 08:30
[2] 15:06
[3] 37:36-37
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Zaad Daa´iyah ila Allaah, uk. 16
- Imechapishwa: 03/11/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)