10. Je, wudhuu´ unachenguka kwa kuisha kwa muda wa kupaka?

Wanazuoni katika hilo wana maono mbalimbali. Yaliyo mashuhuri zaidi katika hayo ni mawili unayoweza kuyapata katika madhehebu ya ash-Shaafi´iy:

1 – Ni wajibu kutawadha upya.

2 – Inamtosheleza kuosha miguu.

3 – Hakuna kinachomlazimu. Twahara yake ni sahihi ataswali nayo maadamu hajapata hadathi. an-Nawawiy (Rahimahu Allaah) amesema:

”Maoni ya tatu ndio yenye nguvu zaidi.”

Maoni hayo yamechaguliwa na an-Nawawiy akienda kinyume na madhehebu yake pia. Akasema (Rahimahu Allaah):

”Maoni haya ameyapokea Ibn-ul-Mundhir kutoka kwa al-Hasan al-Baswriy, Qataadah na Sulaymaan bin Harb na akayachagua Ibn-ul-Mundhir mwenyewe. Nayo ndiyo yaliyochaguliwa yenye nguvu zaidi. Maswahiba zetu wamemnasibishia nayo pia Daawuud.”[1]

[1] al-Majmuu´ (1/527).

  • Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Itmaam-un-Nush fiy Ahkaam-il-Mash, uk. 92
  • Imechapishwa: 27/04/2026