Baadhi ya waliokuwa wanayajua haya wamepingana na Hadiyth:
“Mola Wetu (Tabaarak wa Ta´ala) huteremka katika mbingu ya chini pale kunapobaki theluthi ya mwisho ya usiku na husema: “Ni nani mwenye kuniomba nimuitikie? Ni nani mwenye kuniomba nimpe? Ni nani mwenye kuniomba msamaha nimsamehe?”[1]
na wakasema kuwa theluthi ya usiku inatofautiana kutoka mji mmoja kwenda mwingine – kwa hiyo haiyumkiniki kushuka kukawa wakati maalum.
Ni jambo linalotambulika kihakika ubaya wa upingaji kama huu. Isitoshe Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na makhaliyfah wake waongofu iwapo wangelimsikia mmoja anayepinga namna hiyo, wasingemjadili peke yake bali pia kumuadhibu na kumzingatia mtu huyo ni miongoni mwa wanafiki na wenye kukadhibisha.
[1]al-Bukhaariy (7494) na Muslim (758).
- Muhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn bin Rajab al-Hanbaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bayaan Fadhwl ´Ilm-is-Salaf ´alaa ´Ilm-il-Khalaf, uk. 48
- Imechapishwa: 14/09/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)