Huyu hapa Ibraahiym (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye alikataliwa na watu wake bali wakafikia mpaka kumchafua kati ya watu:
قَالُوا فَأْتُوا بِهِ عَلَىٰ أَعْيُنِ النَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَشْهَدُونَ
“Wakasema: “Mleteni mbele ya macho ya watu ili wapate kushuhudia.””[1]
Kisha wakamtishia kumchoma moto:
قَالُوا حَرِّقُوهُ وَانصُرُوا آلِهَتَكُمْ إِن كُنتُمْ فَاعِلِينَ
“Wakasema: “Mchomeni moto na mnusuru waungu wenu, mkiwa ni wafanyao nusura.””[2]
Wakawasha moto mkubwa na wakamrusha kwa manati kubwa kutokana na kuwa kwao mbali nao kwa sababu ya ukali wake. Lakini Allaah akasema:
قُلْنَا يَا نَارُ كُونِي بَرْدًا وَسَلَامًا عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ
“Tukasema: “Ee moto! Kuwa baridi na salama kwa Ibraahiym!”[3]
Moto ukawa ni wenye baridi iliosalama na akaokoka nao. Hivyo mwisho mwema ukawa kwa Ibraahiym:
وَأَرَادُوا بِهِ كَيْدًا فَجَعَلْنَاهُمُ الْأَخْسَرِينَ
“Wakamkusudia njama, lakini Tukawafanya wao ndio wenye kukhasirika.”[4]
[1] 21:61
[2] 21:68
[3] 21:69
[4] 21:70
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Zaad Daa´iyah ila Allaah, uk. 15
- Imechapishwa: 02/11/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)