06 – Uchumi
Qur-aan imebainisha misingi ya kiuchumi ambayo tanzu zote zinarejea kwayo, mambo ya kiuchumi yarejea katika misingi miwili:
1 – Njia nzuri ya kuchuma pesa.
2 – Njia ya kuzitumia.
Tazama jinsi Kitabu cha Allaah kinavyombainishia mwanadamu namna anavyotakiwa kuchuma pesa kwa njia inayolingana na marua na dini. Amesema:
فَإِذَا قُضِيَتِ الصَّلَاةُ فَانتَشِرُوا فِي الْأَرْضِ وَابْتَغُوا مِن فَضْلِ اللَّـهِ
“Na inapomalizika swalah, basi tawanyikeni katika ardhi na tafuteni fadhilah za Allaah.”[1]
وَآخَرُونَ يَضْرِبُونَ فِي الْأَرْضِ يَبْتَغُونَ مِن فَضْلِ اللَّـهِ
“Na wengine wanasafiri katika ardhi wanatafuta fadhilah za Allaah.”[2]
لَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ أَن تَبْتَغُوا فَضْلًا مِّن رَّبِّكُمْ
“Hapana kwenu dhambi kutafuta fadhilah toka kwa Mola wenu.”[3]
إِلَّا أَن تَكُونَ تِجَارَةً عَن تَرَاضٍ مِّنكُمْ
“… isipokuwa iwe biashara kwa kuridhiana kati yenu.”[4]
وَأَحَلَّ اللَّـهُ الْبَيْعَ
“Allaah amehalalisha biashara.”[5]
فَكُلُوا مِمَّا غَنِمْتُمْ حَلَالًا طَيِّبًا
“Kuleni katika mlivyopata ngawira [hivyo ni] halali vizuri.”[6]
Tazama namna inavyoamrisha utumiaji wa uchumi:
وَلَا تَجْعَلْ يَدَكَ مَغْلُولَةً إِلَىٰ عُنُقِكَ وَلَا تَبْسُطْهَا كُلَّ الْبَسْطِ
“Na wala usifanye mkono wako kama uliofungwa shingoni mwako [kama bakhili] na wala usiukunjue wote kabisa [ukatoa kwa fujo].”[7]
وَالَّذِينَ إِذَا أَنفَقُوا لَمْ يُسْرِفُوا وَلَمْ يَقْتُرُوا وَكَانَ بَيْنَ ذَٰلِكَ قَوَامًا
“Na wale ambao wanapotoa huwa hawafanyi israfu na wala hawafanyi uchoyo na wanakuwa wastani baina ya hayo.”[8]
وَيَسْأَلُونَكَ مَاذَا يُنفِقُونَ قُلِ الْعَفْوَ
“Na wanakuuliza nini watoe. Sema: “Yaliyokuzidieni.””[9]
Tazama namna inavyokataza utumiaji wa haramu:
إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا يُنفِقُونَ أَمْوَالَهُمْ لِيَصُدُّوا عَن سَبِيلِ اللَّـهِ ۚفَسَيُنفِقُونَهَا ثُمَّ تَكُونُ عَلَيْهِمْ حَسْرَةً ثُمَّ يُغْلَبُونَ ۗ وَالَّذِينَ كَفَرُوا إِلَىٰ جَهَنَّمَ يُحْشَرُونَ
“Hakika wale waliokufuru wanatoa mali zao ili wawazuie [watu] kutokamana na njia ya Allaah. Basi watazitoa, kisha itakuwa ni majuto juu yao, kisha watashindwa. Na wale waliokufuru watakusanywa kwenye Moto.”[10]
[1] 62:10
[2] 73:20
[3] 02:198
[4] 04:29
[5] 02:275
[6] 08:69
[7] 17:29
[8] 25:67
[9] 02:219
[10] 08:36
- Muhusika: Imaam Muhammad Amiyn ash-Shanqiytwiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Islaam diyn al-Kaamil, uk. 18-19
- Imechapishwa: 13/06/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)