Swali 06: Ni ipi hukumu ya kukodisha maduka ya biashara kwa wale wanaouza sigara, nyimbo na kanda za video zisokuwa nzuri au benki za ribaa?
Jibu: Hukumu ya kukodisha maduka haya inabainika katika maneno Yake (Ta´ala):
وَتَعَاوَنُوا عَلَى الْبِرِّ وَالتَّقْوَىٰ ۖوَلَا تَعَاوَنُوا عَلَى الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ
“Saidiane katika wema na kumcha Allaah na wala msisaidiane katika dhambi na uadui.”[1]
Kutokana na hili kukodisha maduka kwa ajili ya utumiwaji uliyotajwa katika swali ni haramu. Kwa sababu ni kusaidiana katika dhambi na uadui.
[1] 05:02
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: As-ilah Muhimmah, uk. 14
- Imechapishwa: 26/02/2023