Kuhusu adhabu ni zenye kutofautiana:
1- Za kidunia. Adhabu za kidunia zimegawanyika aina mbili:
A- Zilizowekwa katika Shari´ah kama mfano wa kuuliwa baada ya kunywa kwa mara ya nne, jambo ambalo lina maneno yanayotambulika.
B- Adhabu za kilimwengu kama mfano wa kugeuzwa ngedere na nguruwe na maporomoko ya ardhi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Watakuweko watu katika Ummah wangu ambao watakunywa pombe na ala za muziki zitapigwa juu ya vichwa vyao. Allaah atawadidimiza chini ya ardhi na atawageuza ngedere na nguruwe.”[1]
Miongoni mwa adhabu zipo ambazo ni ndani ya kaburi, tutalitaja huko mbele. Mujaahid amesema:
“Hakuna yeyote anayekufa ilihali ni mzinzi, mwizi au chapombe, isipokuwa Allaah atamwekea ndani ya kaburi lake nyoka wawili wenye pembe wataokuwa wanamuuma hadi siku ya Qiyaamah.”
Sahl bin al-Anbaariy amesema:
“Nilimwendea bwana mmoja ambaye alikuwa anataka kukata roho. Wakati nilipokuwa kwake akapiga makelele na kushika magoti yangu. Akaniogopesha. Nikamwambia: “Una nini wewe?” Akasema: “Kule kuna muhabeshi wa bluu. Macho yake ni kama mapipa. Amenikamata na kunambia: “Mida ya adhuhuri utaenda Motoni.” Baada ya hapo nikauliza ni kipi bwana huyo alikuwa anafanya. Nikapata khabari kwamba alikuwa ni mnywaji mvinyo.”[2]
[1] Ibn Maajah (4020) na Ibn Hibbaan (6758).
[2] Ibn Abiyd-Dunyaa katika ”Kitaab-ul-Muhtadhwariyn”, uk. 164-165
- Muhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn bin Rajab al-Hanbaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Dhamm-ul-Khamr, uk. 14-15
- Imechapishwa: 25/07/2020
Kuhusu adhabu ni zenye kutofautiana:
1- Za kidunia. Adhabu za kidunia zimegawanyika aina mbili:
A- Zilizowekwa katika Shari´ah kama mfano wa kuuliwa baada ya kunywa kwa mara ya nne, jambo ambalo lina maneno yanayotambulika.
B- Adhabu za kilimwengu kama mfano wa kugeuzwa ngedere na nguruwe na maporomoko ya ardhi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Watakuweko watu katika Ummah wangu ambao watakunywa pombe na ala za muziki zitapigwa juu ya vichwa vyao. Allaah atawadidimiza chini ya ardhi na atawageuza ngedere na nguruwe.”[1]
Miongoni mwa adhabu zipo ambazo ni ndani ya kaburi, tutalitaja huko mbele. Mujaahid amesema:
“Hakuna yeyote anayekufa ilihali ni mzinzi, mwizi au chapombe, isipokuwa Allaah atamwekea ndani ya kaburi lake nyoka wawili wenye pembe wataokuwa wanamuuma hadi siku ya Qiyaamah.”
Sahl bin al-Anbaariy amesema:
“Nilimwendea bwana mmoja ambaye alikuwa anataka kukata roho. Wakati nilipokuwa kwake akapiga makelele na kushika magoti yangu. Akaniogopesha. Nikamwambia: “Una nini wewe?” Akasema: “Kule kuna muhabeshi wa bluu. Macho yake ni kama mapipa. Amenikamata na kunambia: “Mida ya adhuhuri utaenda Motoni.” Baada ya hapo nikauliza ni kipi bwana huyo alikuwa anafanya. Nikapata khabari kwamba alikuwa ni mnywaji mvinyo.”[2]
[1] Ibn Maajah (4020) na Ibn Hibbaan (6758).
[2] Ibn Abiyd-Dunyaa katika ”Kitaab-ul-Muhtadhwariyn”, uk. 164-165
Muhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn bin Rajab al-Hanbaliy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Dhamm-ul-Khamr, uk. 14-15
Imechapishwa: 25/07/2020
https://firqatunnajia.com/05-mageuzi-na-maporomoko-ya-ardhi/
Mshirikishe mwenzako:
- Share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Print (Opens in new window) Print
- Email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Share on X (Opens in new window) X
- Share on Pocket (Opens in new window) Pocket