Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
9 – Hafanani na viumbe/watu[1].
10 – Yuhai na hafi, Msimamizi wa kila kitu Asiyelala.
11 – Muumbaji asiyekuwa na haja, mtoaji riziki bila matatizo[2].
12 – Mwenye kufisha bila ya khofu yoyote, Mwenye kufufua bila ya uzito wowote.
[1] Ibn Abiyl-´Izz al-Hanafiy amesema:
“Makusudio sio kukanusha sifa, kama wanavofanya Ahl-ul-Bid´ah. Abu Haniyfah amesema katika “Fiqh-ul-Akbar”:
“Hafanani na chochote katika viumbe Wake na hakuna chochote katika viumbe Wake kinachofanana Naye.”
Kisha baada ya hapo akasema:
“Sifa Zake zote zinatofautiana na sifa za viumbe. Anajua, lakini si kama ujuzi wetu, na Anaweza, lakini si kama uwezo wetu, Anaona, lakini si kama kuona kwetu.” (Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 85)
[2] Si mwenye kuhisi ugumu wala kutilia bidii.
- Muhusika: ´Allaamah Muhammad bin ´Abdil-´Aziyz bin Maaniy´
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Haashiyah ´alaa al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 22
- Imechapishwa: 11/11/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)