Uniangalie pamoja na wale Unaowaangalia – Kwa maana ya kwamba kuwa ni Mlinzi wetu. Kuna aina mbili ya ulinzi (الولاية):
1 – Ulinzi wenye kuenea.
2 – Ulinzi maalum.
Ulinzi maalum unakuwa kwa waumini. Kama alivosema Allaah (Ta´ala):
اللَّـهُ وَلِيُّ الَّذِينَ آمَنُوا يُخْرِجُهُم مِّنَ الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ ۖ وَالَّذِينَ كَفَرُوا أَوْلِيَاؤُهُمُ الطَّاغُوتُ
“Allaah ni mlinzi wa wale ambao wameamini; Anawatoa kutoka katika viza na kuwaingiza katika nuru. Na wale ambao wamekufuru walinzi wao ni Twaaghuut.”[1]
Kwa hivyo unamwomba Allaah ulinzi maalum ambao unapelekea utunzaji kwa yule ambaye Allaah (´Azza wa Jall) anamwangalia na kumuwafikisha katika yale anayoyapenda na kuyaridhia.
Lakini ulinzi wenye kuenea anaingia kila mmoja. Allaah ni mlinzi wa kila mmoja. Kama alivosema Allaah (Ta´ala):
حَتَّىٰ إِذَا جَاءَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ تَوَفَّتْهُ رُسُلُنَا وَهُمْ لَا يُفَرِّطُونَ
”… mpaka kinapomfikia mmoja wenu kifo, basi wajumbe Wetu humfisha, nao hawazembei.”[2]
Hili ni lenye kuenea kwa kila mmoja. Kisha akasema:
ثُمَّ رُدُّوا إِلَى اللَّـهِ مَوْلَاهُمُ الْحَقِّ
”Kisha watarudishwa (wote waliofishwa) kwa Allaah Rabb wao wa haki.”[3]
Lakini wakati tunaomba kwa kusema:
اللهم اجعلنا من أوليائك
”Ee Allaah! Tujaalie kuwa katika wapenzi Wako.”
اللهم تولنا
”Ee Allaah! Tulinde.”
tunakusudia ulinzi maalum ambao unapelekea kutiliwa manani na kuwafikishwa katika yale anayopenda na kuyaridhia.
[1] 02:257
[2] 06:61
[3] 06:62
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Du´aa´ al-Qunuut-il-Witr, uk. 09-10
- Imechapishwa: 09/03/2024
Uniangalie pamoja na wale Unaowaangalia – Kwa maana ya kwamba kuwa ni Mlinzi wetu. Kuna aina mbili ya ulinzi (الولاية):
1 – Ulinzi wenye kuenea.
2 – Ulinzi maalum.
Ulinzi maalum unakuwa kwa waumini. Kama alivosema Allaah (Ta´ala):
اللَّـهُ وَلِيُّ الَّذِينَ آمَنُوا يُخْرِجُهُم مِّنَ الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ ۖ وَالَّذِينَ كَفَرُوا أَوْلِيَاؤُهُمُ الطَّاغُوتُ
“Allaah ni mlinzi wa wale ambao wameamini; Anawatoa kutoka katika viza na kuwaingiza katika nuru. Na wale ambao wamekufuru walinzi wao ni Twaaghuut.”[1]
Kwa hivyo unamwomba Allaah ulinzi maalum ambao unapelekea utunzaji kwa yule ambaye Allaah (´Azza wa Jall) anamwangalia na kumuwafikisha katika yale anayoyapenda na kuyaridhia.
Lakini ulinzi wenye kuenea anaingia kila mmoja. Allaah ni mlinzi wa kila mmoja. Kama alivosema Allaah (Ta´ala):
حَتَّىٰ إِذَا جَاءَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ تَوَفَّتْهُ رُسُلُنَا وَهُمْ لَا يُفَرِّطُونَ
”… mpaka kinapomfikia mmoja wenu kifo, basi wajumbe Wetu humfisha, nao hawazembei.”[2]
Hili ni lenye kuenea kwa kila mmoja. Kisha akasema:
ثُمَّ رُدُّوا إِلَى اللَّـهِ مَوْلَاهُمُ الْحَقِّ
”Kisha watarudishwa (wote waliofishwa) kwa Allaah Rabb wao wa haki.”[3]
Lakini wakati tunaomba kwa kusema:
اللهم اجعلنا من أوليائك
”Ee Allaah! Tujaalie kuwa katika wapenzi Wako.”
اللهم تولنا
”Ee Allaah! Tulinde.”
tunakusudia ulinzi maalum ambao unapelekea kutiliwa manani na kuwafikishwa katika yale anayopenda na kuyaridhia.
[1] 02:257
[2] 06:61
[3] 06:62
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Du´aa´ al-Qunuut-il-Witr, uk. 09-10
Imechapishwa: 09/03/2024
https://firqatunnajia.com/05-aina-mbili-ya-uangalizi-na-ulinzi-wa-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)