Mtunzi amesema:
Dalili ni Kauli Yake (Ta´ala):
مَا كَانَ لِلْمُشْرِكِينَ أَن يَعْمُرُواْ مَسَاجِدَ الله شَاهِدِينَ عَلَى أَنفُسِهِمْ بِالْكُفْرِ أُوْلَئِكَ حَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ وَفِي النَّارِ هُمْ خَالِدُونَ
“Si haki kwa washirikina kuamirisha misikiti ya Allaah hali ya kuwa wanajishuhudia nafsi zao kwa ukafiri. Hao yamebatilika matendo yao na katika Moto wao ni wenye kudumu.”[1]
Mtunzi (Rahimahu Allaah) ametumia dalili kwa Aayah hii ya kwamba matendo yake yote ni yenye kuharibika. Hiyo ina maana kwamba matendo yake yote ni batili na hayalipwi thawabu wala ujira. Miongoni mwa matendo ni swalah. Swalah yake haisihi mpaka ampwekeshe Allaah. Mtunzi amesema:
وَقَدِمْنَا إِلَى مَا عَمِلُوا مِنْ عَمَلٍ فَجَعَلْنَاهُ هَبَاء مَّنثُورًا
”Na Tutayaendea yale waliyoyatenda ya matendo yoyote yale na Tutayafanya kuwa ni mavumbi yaliyotawanyika.”[2]
Dhamiri katika:
إِلَى مَا عَمِلُوا مِنْ عَمَلٍ
“… yale waliyoyatenda ya matendo yoyote yale… “
inarudi kwa makafiri. Amesema (Ta´ala):
فَجَعَلْنَاهُ هَبَاء مَّنثُورًا
“… na Tutayafanya kuwa ni mavumbi yaliyotawanyika.”
Bi maana tutayafanya hayana hukumu wala nafasi yoyote.
Imaam Mujaddid Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amepambanuka kwa njia ya kwamba hataji kitu isipokuwa kwa dalili. Dalili ima ikawa ni Aayah kutoka ndani ya Qur-aan au Hadiyth kutoka katika Sunnah takasifu. Madai hayakubaliwi isipokuwa kwa dalili. Pindi mayahudi waliposema:
لَن يَدْخُلَ الْجَنَّةَ إِلَّا مَن كَانَ هُودًا
“Hatoingia Peponi isipokuwa aliyekuwa myahudi.”
Manaswara nao wakasema:
لَن يَدْخُلَ الْجَنَّةَ إِلَّا مَن كَانَ هُودًا أَوْ نَصَارَىٰ
“Hatoingia Peponi isipokuwa aliyekuwa myahudi au mnaswara.”
Allaah (Ta´ala) akasema:
قُلْ هَاتُوا بُرْهَانَكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
“Sema: “Leteni ushahidi wenu, mkiwa ni wasema kweli.”[3]
[1] 09:17
[2] 25:23
[3] 02:111
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 10-11
- Imechapishwa: 06/12/2021
Mtunzi amesema:
Dalili ni Kauli Yake (Ta´ala):
مَا كَانَ لِلْمُشْرِكِينَ أَن يَعْمُرُواْ مَسَاجِدَ الله شَاهِدِينَ عَلَى أَنفُسِهِمْ بِالْكُفْرِ أُوْلَئِكَ حَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ وَفِي النَّارِ هُمْ خَالِدُونَ
“Si haki kwa washirikina kuamirisha misikiti ya Allaah hali ya kuwa wanajishuhudia nafsi zao kwa ukafiri. Hao yamebatilika matendo yao na katika Moto wao ni wenye kudumu.”[1]
Mtunzi (Rahimahu Allaah) ametumia dalili kwa Aayah hii ya kwamba matendo yake yote ni yenye kuharibika. Hiyo ina maana kwamba matendo yake yote ni batili na hayalipwi thawabu wala ujira. Miongoni mwa matendo ni swalah. Swalah yake haisihi mpaka ampwekeshe Allaah. Mtunzi amesema:
وَقَدِمْنَا إِلَى مَا عَمِلُوا مِنْ عَمَلٍ فَجَعَلْنَاهُ هَبَاء مَّنثُورًا
”Na Tutayaendea yale waliyoyatenda ya matendo yoyote yale na Tutayafanya kuwa ni mavumbi yaliyotawanyika.”[2]
Dhamiri katika:
إِلَى مَا عَمِلُوا مِنْ عَمَلٍ
“… yale waliyoyatenda ya matendo yoyote yale… “
inarudi kwa makafiri. Amesema (Ta´ala):
فَجَعَلْنَاهُ هَبَاء مَّنثُورًا
“… na Tutayafanya kuwa ni mavumbi yaliyotawanyika.”
Bi maana tutayafanya hayana hukumu wala nafasi yoyote.
Imaam Mujaddid Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amepambanuka kwa njia ya kwamba hataji kitu isipokuwa kwa dalili. Dalili ima ikawa ni Aayah kutoka ndani ya Qur-aan au Hadiyth kutoka katika Sunnah takasifu. Madai hayakubaliwi isipokuwa kwa dalili. Pindi mayahudi waliposema:
لَن يَدْخُلَ الْجَنَّةَ إِلَّا مَن كَانَ هُودًا
“Hatoingia Peponi isipokuwa aliyekuwa myahudi.”
Manaswara nao wakasema:
لَن يَدْخُلَ الْجَنَّةَ إِلَّا مَن كَانَ هُودًا أَوْ نَصَارَىٰ
“Hatoingia Peponi isipokuwa aliyekuwa myahudi au mnaswara.”
Allaah (Ta´ala) akasema:
قُلْ هَاتُوا بُرْهَانَكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
“Sema: “Leteni ushahidi wenu, mkiwa ni wasema kweli.”[3]
[1] 09:17
[2] 25:23
[3] 02:111
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 10-11
Imechapishwa: 06/12/2021
https://firqatunnajia.com/04-mfano-wa-namna-ambavo-ibn-abdil-wahhaab-hataji-kitu-isipokuwa-kwa-dalili/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)