3 – Imethibiti kwa al-Bukhaariy na Muslim kupitia kwa Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ambaye amesimulia:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alifunga ´Aashuuraa´ na akaamrisha kuifunga. Wakati kulipofaradhishwa Ramadhaan ikaachwa.”[1]
Maneno yake:
“… ikaachwa.”
Bi maana ikaachwa swawm ya ´Aashuuraa´ hali ya kuwa lazima na kukabakia kule kupendezwa kwake. Haafidh Ibn Hajar amesema:
“Hakukuachwa kule kupendekezwa kwake. Ni kitu kilichobakia. Ikafahamisha kuwa kilichoachwa ni ule ulazima wake.”[2]
al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kupitia kwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ambaye amesimulia:
“Quraysh walikuwa wakifunga siku ya ´Aashuuraa´ kabla ya kuja Uislamu. Kisha Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaamrisha kuifunga mpaka ilipofaradhishwa Ramadhaan. Ndipo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema:
“Mwenye kutaka kuifunga aifunge na mwenye kutaka ale.”[3]
[1] al-Bukhaariy (1892).
[2] Fath-ul-Baariy (04/237).
[3] al-Bukhaariy (1893) na Muslim (1125).
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ilmaam bishay´ min Ahkaam-is-Swiyaam, uk. 11
- Imechapishwa: 26/03/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)