1- Ukuu wa akilii ni kutambua matukio yaliyo njiani kabla hayajatokea.
2- Ni wajibu kwa mwenye busara kujiepusha na mambo matatu yanayoiharibu akili haraka kuliko moto unavyounguza majani makavu; kucheka kwa kipindukia, kuwa na matumaini mengi mabaya na mathibitisho mabaya.
3- Mwenye busara hujitolea kwa rafiki yake nafsi na mali yake, maarifa yake na uwepo wake na wema wake na ambaye si msomi bishara yake na mamkazi yake.
4- Aliye na busara hachukui msaada isipokuwa kwa yule anayejua kuwa atamsaidia. Hazungumzi isipokuwa tu na yule ambaye anaona maneno yake ni yenye faida isipokuwa kutapokuwa kuna dharurah ya kufanya hivo.
5- Fadhila za watu hazipatikani katika madai yao wenyewe. Zinapatikana katika yale watu wanayowanasibishia. Mwenye busara hajali mambo ya kidunia yaliyompita akilinganisha na ile akili aliyotunukiwa.
6- Aliye na busara hatamani kile asichokipata na wala halimbikizi pindi anapopata.
7- Mwenye busara anaheshimiwa pasi na pesa kama jinsi simba inavyoogopwa ingawa imelala.
8- Maneno ya mwenye busara ni ya sawa kama mwili wa aliye na afya njema na maneno ya mjinga ni yenye kujigonga kama mchanganyiko kwenye mwili wa mgonjwa.
9- Hata kama maneno ya mwenye busara yatakuwa mafupi, ni yenye thamani kubwa. Hata kama machafu ya mtenda dhambi ni madogo, ni msiba wa wazi.
10- Ni katika busara mtu kuthibitisha kwanza kabla ya kufanya kitendo chochote.
11- Ugonjwa wa busara ni kujiona. Ni juu ya mwenye busara kuwa na ustahamilivu kwa jirani muovu, jamaa waovu na matangamano maovu. Hatowaepuka jinsi siku zinavyokwenda.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Hibbaan al-Bustiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Rawdhat-ul-´Uqalaa’ wa Nuzhat-ul-Fudhwalaa’, uk. 23-24
- Imechapishwa: 13/10/2016
1- Ukuu wa akilii ni kutambua matukio yaliyo njiani kabla hayajatokea.
2- Ni wajibu kwa mwenye busara kujiepusha na mambo matatu yanayoiharibu akili haraka kuliko moto unavyounguza majani makavu; kucheka kwa kipindukia, kuwa na matumaini mengi mabaya na mathibitisho mabaya.
3- Mwenye busara hujitolea kwa rafiki yake nafsi na mali yake, maarifa yake na uwepo wake na wema wake na ambaye si msomi bishara yake na mamkazi yake.
4- Aliye na busara hachukui msaada isipokuwa kwa yule anayejua kuwa atamsaidia. Hazungumzi isipokuwa tu na yule ambaye anaona maneno yake ni yenye faida isipokuwa kutapokuwa kuna dharurah ya kufanya hivo.
5- Fadhila za watu hazipatikani katika madai yao wenyewe. Zinapatikana katika yale watu wanayowanasibishia. Mwenye busara hajali mambo ya kidunia yaliyompita akilinganisha na ile akili aliyotunukiwa.
6- Aliye na busara hatamani kile asichokipata na wala halimbikizi pindi anapopata.
7- Mwenye busara anaheshimiwa pasi na pesa kama jinsi simba inavyoogopwa ingawa imelala.
8- Maneno ya mwenye busara ni ya sawa kama mwili wa aliye na afya njema na maneno ya mjinga ni yenye kujigonga kama mchanganyiko kwenye mwili wa mgonjwa.
9- Hata kama maneno ya mwenye busara yatakuwa mafupi, ni yenye thamani kubwa. Hata kama machafu ya mtenda dhambi ni madogo, ni msiba wa wazi.
10- Ni katika busara mtu kuthibitisha kwanza kabla ya kufanya kitendo chochote.
11- Ugonjwa wa busara ni kujiona. Ni juu ya mwenye busara kuwa na ustahamilivu kwa jirani muovu, jamaa waovu na matangamano maovu. Hatowaepuka jinsi siku zinavyokwenda.
Muhusika: Imaam Muhammad bin Hibbaan al-Bustiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Rawdhat-ul-´Uqalaa’ wa Nuzhat-ul-Fudhwalaa’, uk. 23-24
Imechapishwa: 13/10/2016
https://firqatunnajia.com/03-ukuu-wa-akili-ni-kutambua-matukio-kabla-hayajatokea/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)