2 – Kuamini kwa kukata na kusadikisha ya kwamba Allaah yuko na majina mazuri na sifa tukufu na kuu. Majina hayo Mola amejiita nayo Mwenyewe au amemuita nayo Mtume Wake, na Mola amejisifu kwayo au amesifiwa kwayo na Mtume Wake. Mfano wa majina hayo ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona, Mjuzi, Muweza, Mwingi wa huruma, Mwenye kurehemu. Mfano wa sifa hizo ni ujuzi, uwezo, huruma, kuridhia, kughadhibika na nyenginezo. Ni lazima kuitakidi na kuamini kuwa majina na sifa hizi ni za kikweli. Ni sifa za kikweli ambazo zinalingana na utukufu na ukubwa Wake. Kwa maana nyingine hazilingana na majina na sifa za viumbe. Ni sifa na majina ya kweli. Kwa msemo mwingine haitakiwi kuzipotosha, kuzikanusha, kuzifanyia namna wala kuzilinganisha. Hivi ndivo anavyopwekeshwa Mola kwa majina na sifa Zake. Hii ndio huitwa Tawhiyd-ul-Asmaa´ was-Swifaat.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Iymaan – Haqiyqatuhu wa Nawaaqidhwuh, uk. 07-08
- Imechapishwa: 20/03/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)