Kuhusu ni nani ambaye anawajibika kufunga? Ni yule ambaye ´ibaadah inamuwajibikia kwa namna ya kwamba kumethubutu kwake sharti zifuatazo:
1 – Uislamu. Kwa msemo mwingine ni kwamba swawm haisihi kutoka kwa kafiri katika hali ya ukafiri wake. Ikitokea amefunga, haisihi wala kukubaliwa kutoka kwake. Amesema (Ta´ala):
وَمَا مَنَعَهُمْ أَن تُقْبَلَ مِنْهُمْ نَفَقَاتُهُمْ إِلَّا أَنَّهُمْ كَفَرُوا بِاللَّـهِ وَبِرَسُولِهِ
”Haikuwazuilia kukubaliwa michango yao isipokuwa kwa kuwa wao walimkufuru Allaah na Mtume Wake.”[1]
Kafiri anazungumzishwa misingi ya ´Aqiydah kwa mujibu wa maafikiano ya wanazuoni[2]. Je, anawajibika pia na matawi ya Shari´ah? Wanazuoni wanatofautiana katika suala hili kwenye maoni mawili:
1 – Makafiri ni wenye kuzungumzishwa matawi ya Shari´ah na watafanyiwa hesabu kwa jambo hilo, jambo ambalo ndio maoni ya kikosi kikubwa cha wanazuoni[3]. Dalili ya hilo ni maneno Yake (Ta´ala):
مَا سَلَكَكُمْ فِي سَقَرَ قَالُوا لَمْ نَكُ مِنَ الْمُصَلِّينَ
“Nini kilichokuingizeni katika [Moto wa] Saqar?” Watasema: “Hatukuwa miongoni mwa wanaoswali.”[4]
2 – Si wenye kuzungumzishwa matawi ya Shari´ah. Haya ni maoni ya Hanafiyyah (Rahimahumu Allaah)[5].
[1] 09:54
[2] al-Furuuq (01/222) na ”al-Ibhaaj” (01/176-177) ya as-Subkiy.
[3] Sharh Tanqiyh-ul-Fusuwl, uk. 162, ”al-Burhaan fiy Usuwl-il-Fiqh” (01/17) na ”Sharh Mukhtaswar-ir-Rawdhwah” (01/205).
[4] 74:42-43
[5] al-Ikhtiyaar lita´liyl-il-Mukhtaar (03/111).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Taysiyr Dhil-In´am bisharh ´Umdat-il-Ahkaam (01/432-433)
- Imechapishwa: 13/02/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)