Allaah (Subhaanah) amewajibisha Ummah huu uwe na kikosi cha watu kinacholingania kwa Allaah (Ta´ala), kinachowaelekeza watu katika kheri, kinawaamrisha mema na kuwatahadharisha na kuwakataza shari. Amesema (Ta´ala):
وَلْتَكُن مِّنكُمْ أُمَّةٌ يَدْعُونَ إِلَى الْخَيْرِ وَيَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ ۚوَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ
“Wawepo kutoka kwenu watu wanaolingania kheri na kuamrisha mema na unaokataza maovu. Hao ndio waliofaulu.”[1]
ادْعُ إِلَىٰ سَبِيلِ رَبِّكَ بِالْحِكْمَةِ وَالْمَوْعِظَةِ الْحَسَنَةِ ۖ وَجَادِلْهُم بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ
“Lingania katika njia ya Mola wako kwa hekima na mawaidha mazuri na jadiliana nao kwa ambayo ni mazuri zaidi.”[2]
Kutokana na Aayah hizi tukufu wanazuoni wamethibitisha kwamba kulingania kwa Allaah (Ta´ala) ni faradhi kwa baadhi ya waislamu. Katika kila zama na mahali ni lazima kuwepo kikundi cha waislamu kinacholingania; asipokuweko yeyote anayesimamia kazi hiyo basi wanapata dhambi wote.
[1] 3:104
[2] 16:125
- Muhusika: Shaykh ´Abdus-Salaam bin Barjas Aal ´Abdil-Kariym
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Hujaj al-Qawiyyah ´alaa anna Wasaa-il-ad-Da´wah Tawqiyfiyyah, uk. 8
- Imechapishwa: 28/07/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)