2 – Madhambi ambayo kuna kujitenga mbali. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema ni pamoja na:

“Yule mwenye kutughushi basi si katika sisi.”[1]

“Si katika sisi yule mwenye kubeba silaha dhidi yetu.”[2]

 “Si katika sisi yule asiyewahurumia wadogo wetu.”[3]

[1] Muslim (101) kupitia kwa Abu Hurayrah kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa tamko lisemalo:

“Yule mwenye kubeba silaha dhidi yetu si katika sisi, na yule mwenye kutughushi si katika sisi.”

Yeye pia ndiye ambaye amepokea sehemu yake ya kwanza kupitia kwa Ibn ´Umar na Abu Muusa.

[2] Muslim (101).

[3] Ahmad kupitia kwa Ibn ´Umar kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). al-Haakim ameisahihisha kwa mujibu wa sharti za Muslim na adh-Dhahabiy akaafikiana naye.

  • Mhusika: Imaam Abu ´Ubayd al-Qaasim bin Sallaam
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-ul-Iymaan, uk. 70
  • Imechapishwa: 29/06/2023
  • taaliki: Imaam Muhammad Naawswir-ud-Diyn al-Albaaniy