02. Hadiyth ”Hakika mimi naona unapenda kondoo na mashamba…. “

232 – ´Abdullaah bin ´Abdir-Rahmaan bin Abiy Swa´swa´h amesimulia kwamba Abu Sa´iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ´anh) alimwambia:

“Hakika mimi naona unapenda wanyamahoa na mashamba. Unapokuwa na kondoo wako au shambani mwako na ukaadhini kwa ajili ya swalah, basi nyanyua sauti yako wakati wa kuita. Kwa sababu hakuna jini, mtu au kitu kingine kinachosikia sauti ya muadhini ispokuwa kitamtolea ushuhuda siku ya Qiyaamah. Nimeyasikia hayo kutoka kwa Allaah wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”[1]

Ameipokea Maalik, al-Bukhaariy, an-Nasaa´iy na Ibn Maajah ambaye amezidisha:

“… wala jiwe wala mti isipokuwa utamtolea ushuhuda.”

Ibn Khuzaymah ameipokea katika “as-Swahiyh” yake ambaye amesimulia kuwa amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:

“Hakuna mti, udongo, jini wala mtu anayesikia sauti yake isipokuwa vitamtolea ushuhuda.”[2]

[1] Swahiyh.

[2] Swahiyh.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/212)
  • Imechapishwa: 21/02/2022
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy