Kwa ajili hiyo nasema:
Ametakasika na mapungufu Yule anayewajaribu watu
Anaowapenda – mtihani ni zawadi
Subiri kwa mtihani na kuwa ni mwenye kuridhia
hiyo ndio dawa
Jisalimishe kwa Allaah yale aliyohukumu –
na Allaah anayafanya ayatakayo
Tanzia ni Sunnah kubwa na ni sifa inayopendeza na inayoridhiwa. Sijaona tanzia ilio kubwa zaidi kwa aliyefikwa na msiba kuliko Kitabu kilicho na Aayah za Qur-aan kilichoambatana na khabari, maneno, simulizi na mashairi. Kwa ajili hiyo nikakusanya yale niliyowahi na vyanzo na uanishaji uliyotajwa, kwenda kwa yule anayelengwa na kila ambaye amefikwa na msiba iwe ni faraja na uokozi, pia nishirikiane na aliyefikwa na msiba katika thawabu na wema wake. ´Abdullaah bin Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Yule mwenye kumpa rambirambi aliyefikwa na msiba, basi anapata mfano wa ujira wake.”[1]
Ameipokea at-Tirmidhiy, Ibn Maajah na wengineo.
´Amr bin Hamz (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Hakuna muumini yeyote anayempa pole ndugu yake kutokana na msiba uliyompata isipokuwa Allaah (´Azza wa Jall) humvisha vazi la heshima siku ya Qiyaamah.”[2]
Ameipokea Ibn Maajah.
Kumepokelewa mfano wa hayo kutoka kwa Abu Hurayrah, Abu Barzah al-Aslamiy, Jaabir na wengineo (Radhiya Allaahu ´anhum).
[1] at-Tirmidhiy (1073) na Ibn Maajah (1602). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Dhwa´iyf at-Tirmidhiy” (1073).
[2] Ibn Maajah (1601). Nzuri kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh Sunan Ibn Maajah” (1311).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin ´Abdillaah bin Naaswir-id-Diyn ad-Dimashqiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bard-ul-Akbaad ´inda Faqd-il-Awlaad, uk. 28-30
- Imechapishwa: 08/08/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)