Mlango wa tano: I´tikaaf na kuna masuala yafuatayo:
Suala la kwanza: Maana ya I´tikaaf na hukumu yake
1- Maana
I´tikaaf maana yake kilugha ni kulazimiana na kitu na kuizuia nafsi juu yake.
Maana yake kidini ni muislamu kulazimiana na msikiti kwa ajili ya kumtii Allaah (´Azza wa Jall).
2- Hukumu
Ni Sunnah na kumwabudu Allaah (Ta´ala). Amesema (´Azza wa Jall):
وَعَهِدْنَا إِلَىٰ إِبْرَاهِيمَ وَإِسْمَاعِيلَ أَن طَهِّرَا بَيْتِيَ لِلطَّائِفِينَ وَالْعَاكِفِينَ وَالرُّكَّعِ السُّجُودِ
“Tulichukua ahadi kwa Ibraahiym na Ismaa’iyl kwamba waisafishe Nyumba Yangu kwa wanaotufu na wanaofanya i’tikaaf na wanaorukuu na kusujudu.”[1]
Aayah hii ni dalili juu ya usuniwaji wake mpaka kwa nyumati zilizotangulia. Amesema (Ta´ala):
وَلَا تُبَاشِرُوهُنَّ وَأَنتُمْ عَاكِفُونَ فِي الْمَسَاجِدِ
“Na wala msichanganyike nao hali ya kuwa nyinyi ni wenye kukaa I’tikaaf misikitini.”[2]
´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akikaa I´tikaaf zile siku kumi za mwisho za Ramadhaan mpaka Allaah alipomfisha[3].
Waislamu wameafikiana juu ya usuniwaji wake na kwamba na kwamba ni jambo lililopendekezwa. Haimlazimu mtu isipokuwa pale atakapojiwajibishia mwenyewe kama vile aweke nadhiri. Kwa msemo mwingine ni kwamba usuniwaji wa I´tikaaf umethibiti kwa Qur-aan, Sunnah na maafikiano.
[1] 02:125
[2] 02:187
[3] al-Bukhaariy (2020) na Muslim (1172).
- Mhusika: Nukhbatin minal-´Ulamaa´
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fiqh-ul-Muyassar, uk. 167
- Imechapishwa: 30/04/2021
Mlango wa tano: I´tikaaf na kuna masuala yafuatayo:
Suala la kwanza: Maana ya I´tikaaf na hukumu yake
1- Maana
I´tikaaf maana yake kilugha ni kulazimiana na kitu na kuizuia nafsi juu yake.
Maana yake kidini ni muislamu kulazimiana na msikiti kwa ajili ya kumtii Allaah (´Azza wa Jall).
2- Hukumu
Ni Sunnah na kumwabudu Allaah (Ta´ala). Amesema (´Azza wa Jall):
وَعَهِدْنَا إِلَىٰ إِبْرَاهِيمَ وَإِسْمَاعِيلَ أَن طَهِّرَا بَيْتِيَ لِلطَّائِفِينَ وَالْعَاكِفِينَ وَالرُّكَّعِ السُّجُودِ
“Tulichukua ahadi kwa Ibraahiym na Ismaa’iyl kwamba waisafishe Nyumba Yangu kwa wanaotufu na wanaofanya i’tikaaf na wanaorukuu na kusujudu.”[1]
Aayah hii ni dalili juu ya usuniwaji wake mpaka kwa nyumati zilizotangulia. Amesema (Ta´ala):
وَلَا تُبَاشِرُوهُنَّ وَأَنتُمْ عَاكِفُونَ فِي الْمَسَاجِدِ
“Na wala msichanganyike nao hali ya kuwa nyinyi ni wenye kukaa I’tikaaf misikitini.”[2]
´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akikaa I´tikaaf zile siku kumi za mwisho za Ramadhaan mpaka Allaah alipomfisha[3].
Waislamu wameafikiana juu ya usuniwaji wake na kwamba na kwamba ni jambo lililopendekezwa. Haimlazimu mtu isipokuwa pale atakapojiwajibishia mwenyewe kama vile aweke nadhiri. Kwa msemo mwingine ni kwamba usuniwaji wa I´tikaaf umethibiti kwa Qur-aan, Sunnah na maafikiano.
[1] 02:125
[2] 02:187
[3] al-Bukhaariy (2020) na Muslim (1172).
Mhusika: Nukhbatin minal-´Ulamaa´
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fiqh-ul-Muyassar, uk. 167
Imechapishwa: 30/04/2021
https://firqatunnajia.com/01-mapendekezo-ya-itikaad-na-hukumu-yake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)