Kupitia tafiti za kiusomi za Qur-aan imepata kujulikana kuwa kuna aina tatu za Tawhiyd:
1 – Kumpwekesha Allaah katika uola Wake.
Aina hii ya Tawhiyd inakubaliwa na maumbile ya mtu mwerevu. Amesema (Ta´ala):
وَلَئِن سَأَلْتَهُم مَّنْ خَلَقَهُمْ لَيَقُولُنَّ اللَّـهُ
“Ukiwauliza: “Ni nani kawaumba?” Bila shaka watasema: “Ni Allaah.””[1]
قُلْ مَن يَرْزُقُكُم مِّنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ أَمَّن يَمْلِكُ السَّمْعَ وَالْأَبْصَارَ وَمَن يُخْرِجُ الْحَيَّ مِنَ الْمَيِّتِ وَيُخْرِجُ الْمَيِّتَ مِنَ الْحَيِّ وَمَن يُدَبِّرُ الْأَمْرَ ۚ فَسَيَقُولُونَ اللَّـهُ ۚ فَقُلْ أَفَلَا تَتَّقُونَ
“Sema: “Nani anayekuruzukuni kutoka mbinguni na ardhini au nani anayemiliki kusikia na kuona na nani anayemtoa aliye hai kutoka maiti na anayemtoa maiti kutoka aliye uhai na nani anayeendesha mambo?” Watasema: “Ni Allaah”. Basi sema: “Je, basi hamumchi?”[2]
Pindi Fir´awn alipokanusha aina hii pale aliposema:
وَمَا رَبُّ الْعَالَمِينَ
“Ni nani huyo Mola wa walimwengu?”[3]
alifanya hivo tu kwa sababu ya kiburi na kujifanya ni hamnazo. Dalili ya hilo ni maneno Yake (Ta´ala):
لَقَدْ عَلِمْتَ مَا أَنزَلَ هَـٰؤُلَاءِ إِلَّا رَبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ بَصَائِرَ
“Hakika umekwishajua kwamba hakuna aliyeteremsha haya isipokuwa Mola wa mbingu na ardhi kuwa ni ushahidi wa kuonekana.”[4]
وَجَحَدُوا بِهَا وَاسْتَيْقَنَتْهَا أَنفُسُهُمْ ظُلْمًا وَعُلُوًّا
“Wakazikanusha kwa dhuluma na kujivuna na hali kuwa nafsi zao zimeziyakinisha.”[5]
Kwa ajili hiyo Qur-aan ilikuwa ikishuka kwa njia ya kuthibitisha aina hii ya Tawhiyd kupitia vitu vyenye kuthibitishwa. Mfano wa hilo ni maneno Yake (Ta´ala):
أَفِي اللَّـهِ شَكٌّ
“Je, kuna shaka kuhusiana na Allaah.”[6]
قُلْ أَغَيْرَ اللَّـهِ أَبْغِي رَبًّا وَهُوَ رَبُّ كُلِّ شَيْءٍ
“Sema: “Je, nishike Mola mwingine asiyekuwa Allaah hali ya kuwa Yeye ni Mola wa kila kitu?””[7]
قُلْ مَن رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ قُلِ اللَّـهُ
“Sema: “Ni nani Mola wa mbingu na ardhi?” Sema: “Ni Allaah.””[8]
Hata hivyo aina hii ya Tawhiyd haikuwanufaisha makafiri kitu, kwa sababu hawakuwa wakimuabudu Allaah (Jalla wa ´Alaa) peke yake. Amesema (Ta´ala):
وَمَا يُؤْمِنُ أَكْثَرُهُم بِاللَّـهِ إِلَّا وَهُم مُّشْرِكُونَ
“Na wengi kati yao hawamwamini Allaah isipokuwa ni washirikina.”[9]
مَا نَعْبُدُهُمْ إِلَّا لِيُقَرِّبُونَا إِلَى اللَّـهِ زُلْفَىٰ
“Hatuwaabudu isipokuwa ili watukurubishe kwa Allaah ukaribio.”[10]
وَيَقُولُونَ هَـٰؤُلَاءِ شُفَعَاؤُنَا عِندَ اللَّـهِ
“Wanasema: “Hawa ni waombezi wetu mbele ya Allaah.””[11]
[1] 43:87
[2] 10:31
[3] 26:23
[4] 17:102
[5] 27:14
[6] 14:10
[7] 06:164
[8] 13:16
[9] 12:106
[10] 39:03
[11] 10:18
- Muhusika: Imaam Muhammad Amiyn ash-Shanqiytwiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Islaam diyn al-Kaamil, uk. 8-9
- Imechapishwa: 13/06/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)