205 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
لولا أنْ أَشُقَّ على أُمتي لأمرتُهم بالسِّواك مع كلِّ صلاةٍ
“Lau kama sio kuwatia uzito ummah wangu, basi ningeliwaamrisha kutumia Siwaak wakati wa kila wudhuu´.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy, ambaye tamko ni lake, na kwa Muslim imekuja:
لولا أنْ أَشُقَّ على أُمتي لأمرتُهم بالسِّواك عند كل صلاة
“Lau kama sio kuwatia uzito ummah wangu, basi ningeliwaamrisha kutumia Siwaak wakati wa kila swalah.”
Kwa an-Nasaa´iy, Ibn Maajah na Ibn Hibbaan katika “as-Swahiyh” imekuja:
لولا أنْ أَشُقَّ على أُمتي لأمرتُهم بالسِّواك مع الوضوء عند كل صلاة
“Lau kama sio kuwatia uzito ummah wangu, basi ningeliwaamrisha kutumia Siwaak na kutawadha wakati wa kila swalah.”[2]
Ahmad na Ibn Khuzaymah wameipokea katika ”as-Swahiyh” yake:
لولا أنْ أَشُقَّ على أُمتي لأمرتُهم بالسِّواك مع كلِّ وضُوءٍ
“Lau kama sio kuwatia uzito ummah wangu, basi ningeliwaamrisha kutumia Siwaak wakati wa kila wudhuu´.”[3]
[1] Swahiyh.
[2] Nzuri na Swahiyh.
[3] Swahiyh.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/202)
- Imechapishwa: 05/01/2024
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket