Swali: Kuhusu masuala ya Basmalah wakati wa wudhuu´ Imaam Ahmad amesema “Hakukuthibiti juu ya hilo kitu”. Je, hii ina maana ya kwamba ni sahihi kutawadha bila ya kusema “Bismi Allaah”?
Jibu: Kwa mujibu wa Imaam Ahmad, Basmalah ni wajibu miongoni mwa mambo ya wajibu ya wudhuu´. Kwa kauli yake:
“Hana wudhuu´ yule ambaye hakutaja Jina la Allaah juu yake.”
Kauli ya Imaam Ahmad “Hakukuthibiti juu ya hilo kitu”, yaani hakuna mapokezi sahihi juu ya hilo. Lakini kumepokelewa Hadiyth nyingi dhaifu ambazo zinapeana nguvu. Imaam Ahmad hakusema “Hakukupokelewa juu ya hilo kitu”, bali amesema “Hakukuthibiti”, bi maana hakukusihi juu yake kitu. Hadiyth dhaifu zikiwa nyingi zinapeana nguvu. Kwa ajili hiyo ndio maana Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) ameonelea kuwa ni wajibu kuleta Tasmiyah wakati mtu atapokumbuka. Ama akisahau, wudhuu´ wake ni sahihi.
Wanachuoni wengi wanaonelea kuwa kusema “Bismillaah” kabla ya kuanza kutawadha ni Sunnah na sio wajibu.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (69) http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13888
- Imechapishwa: 16/11/2014
Swali: Kuhusu masuala ya Basmalah wakati wa wudhuu´ Imaam Ahmad amesema “Hakukuthibiti juu ya hilo kitu”. Je, hii ina maana ya kwamba ni sahihi kutawadha bila ya kusema “Bismi Allaah”?
Jibu: Kwa mujibu wa Imaam Ahmad, Basmalah ni wajibu miongoni mwa mambo ya wajibu ya wudhuu´. Kwa kauli yake:
“Hana wudhuu´ yule ambaye hakutaja Jina la Allaah juu yake.”
Kauli ya Imaam Ahmad “Hakukuthibiti juu ya hilo kitu”, yaani hakuna mapokezi sahihi juu ya hilo. Lakini kumepokelewa Hadiyth nyingi dhaifu ambazo zinapeana nguvu. Imaam Ahmad hakusema “Hakukupokelewa juu ya hilo kitu”, bali amesema “Hakukuthibiti”, bi maana hakukusihi juu yake kitu. Hadiyth dhaifu zikiwa nyingi zinapeana nguvu. Kwa ajili hiyo ndio maana Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) ameonelea kuwa ni wajibu kuleta Tasmiyah wakati mtu atapokumbuka. Ama akisahau, wudhuu´ wake ni sahihi.
Wanachuoni wengi wanaonelea kuwa kusema “Bismillaah” kabla ya kuanza kutawadha ni Sunnah na sio wajibu.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (69) http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13888
Imechapishwa: 16/11/2014
https://firqatunnajia.com/ufafanuzi-wa-maneno-ya-imaam-ahmad-kuhusu-basmalah-wakati-wa-wudhuu__trashed/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)