Kufunga masiku meupe ni lazima iwe tarehe 13, 14 na 15?

Swali: Nikitaka kufunga siku tatu kila mwezi ni lazima iwe masiku meupe?

Jibu: Hapana. Funga siku tatu kila mwezi, sawa ikiwa kwa kufuatanisha, mbalimbali na kadhalika. Muhimu ufunge siku tatu kila mwezi, sawa ikiwa ni katika yale masiku meupe au siku zingine. Hakuna neno sawa ikiwa ni mwanzo wa mwezi, katikati yake au mwisho wake.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/eg–14340421.mp3
  • Imechapishwa: 20/09/2020