Swali: Je, inafaa kwa mume kumjamii mke wake mara mbili pasi na kuoga kati ya mfano wa randi ya kwanza, ya pili na ya tatu?
Jibu: Inafaa kwake kufanya hivo licha ya kwamba bora ni kuoga. Imepokelewa kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yanayojulisha juu ya kufanywa na kuachwa kwake. Watunzi wa as-Sunan na Ahmad wamepokea kupitia kwa Raafiy´ bin Khadiyj kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) usiku mmoja aliwazungukia wakeze ambapo anaoga kwa huyu na huyu. Kukasemwa: “Ee Mtume wa Allaah! Kwa nini usifanye josho moja?” Akasema:
“Hivi ndivo takasifu na vizuri zaidi.”
al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kupitia kwa Anas (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesimulia kwamba yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiwazungukia wakeze kwa josho moja.
Sunnah ni kwamba anapotaka kurudia kufanya tendo la ndoa bila kuoga basi angalau atawadhe wudhuu´ kama wa swalah. Pia kumepokelewa yanayojulisha juu ya kuacha kutawadha. Yanayofahamisha juu ya usuniwaji wake ni yale aliyopokea Muslim na wengineo kupitia kwa Abu Sa´iyd (Radhiya Allaahu ´anh) aliyeeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atapomwendea mmoja wenu mke wake kisha akataka kurudia, basi atawadhe.”
Imekuja katika upokezi wa Ibn Khuzaymah:
“Atapomwendea mmoja wenu mke wake kisha akataka kurudia, basi atawadhe wudhuu´ wa swalah.”
Kuhusu yanayojulisha kuacha ni yale aliyopokea at-Twahaawiy kupitia kwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ambaye amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akijamii kisha anarudia na wala hatawadhi.”
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/187)
- Imechapishwa: 29/08/2021
Swali: Je, inafaa kwa mume kumjamii mke wake mara mbili pasi na kuoga kati ya mfano wa randi ya kwanza, ya pili na ya tatu?
Jibu: Inafaa kwake kufanya hivo licha ya kwamba bora ni kuoga. Imepokelewa kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yanayojulisha juu ya kufanywa na kuachwa kwake. Watunzi wa as-Sunan na Ahmad wamepokea kupitia kwa Raafiy´ bin Khadiyj kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) usiku mmoja aliwazungukia wakeze ambapo anaoga kwa huyu na huyu. Kukasemwa: “Ee Mtume wa Allaah! Kwa nini usifanye josho moja?” Akasema:
“Hivi ndivo takasifu na vizuri zaidi.”
al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kupitia kwa Anas (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesimulia kwamba yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiwazungukia wakeze kwa josho moja.
Sunnah ni kwamba anapotaka kurudia kufanya tendo la ndoa bila kuoga basi angalau atawadhe wudhuu´ kama wa swalah. Pia kumepokelewa yanayojulisha juu ya kuacha kutawadha. Yanayofahamisha juu ya usuniwaji wake ni yale aliyopokea Muslim na wengineo kupitia kwa Abu Sa´iyd (Radhiya Allaahu ´anh) aliyeeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atapomwendea mmoja wenu mke wake kisha akataka kurudia, basi atawadhe.”
Imekuja katika upokezi wa Ibn Khuzaymah:
“Atapomwendea mmoja wenu mke wake kisha akataka kurudia, basi atawadhe wudhuu´ wa swalah.”
Kuhusu yanayojulisha kuacha ni yale aliyopokea at-Twahaawiy kupitia kwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ambaye amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akijamii kisha anarudia na wala hatawadhi.”
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (10/187)
Imechapishwa: 29/08/2021
https://firqatunnajia.com/kufanya-jimaa-mara-nyingi-bila-kutawadha-baina-yake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)