Swali: Ikiwa hizi Anaashiyd zimesalimika kutokamana na shirki mfano wake, maneno yako kusema kuwa hazifai yana maana kwamba ni haramu au zimechukizwa tu?

Jibu: Kwangu hakuna kitu kinachoitwa Bid´ah iliyochukizwa au Bid´ah iliyoharamishwa. Kila Bid´ah ni upotofu na kila upotofu ni Motoni. Muhimu ni kwanza mtu aanze kuamini msingi huu unaosapotiwa na Hadiyth nyingi kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kwamba kila Bid´ah ni upotofu na kila upotofu ni Motoni. Aidha atambue kwamba ikiwa Salaf hawakufanya kitendo fulani basi hakuna umuhimu wa kujua kuwa ni haramu au imechukizwa; kila Bid´ah ni upotofu na kila upotofu ni Motoni.

  • Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Silsilat-ul-Hudaa wan-Nuur (158)
  • Imechapishwa: 16/12/2020