an-Najmiy kuhusu idadi ya Khutbah siku ya ´iyd

Swali: Je imethibiti ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa anakhutubu siku ya ´iyd Khutbah mbili?

Jibu: Sijui kuwa alikuwa anakhutubu Khutbah mbili. Isipokuwa tu baada ya kuwakhutubia wanaume alienda kuwakhutubia wanawake. Na hili halichukuliwi kuwa ni Khutbah mbili, kwa kuzingatia ya kwamba wanaume wana Khutbah yao na wanawake wana Khutbah yao.

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alnajmi.net/voices.php?action=show&id=167
  • Imechapishwa: 30/07/2020