Shaykh-ul-Islaam na Imaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Nguzo ya kwanza ni kusimama kwa mwenye kuweza. Dalili ni Kauli Yake (Ta ´ala):
حَافِظُوا عَلَى الصَّلَوَاتِ وَالصَّلَاةِ الْوُسْطَىٰ وَقُومُوا لِلَّـهِ قَانِتِينَ
”Zichungeni swalah na khaswa khaswa swalah ya katikati na simameni mbele ya Allaah hali ya kuwa ni wanyenyekevu.”[1]
MAELEZO
Kuhusiana na kusimama kwa mwenye kuweza, Allaah (Ta´ala) amesema:
وَقُومُوا لِلَّـهِ قَانِتِينَ
”… simameni mbele ya Allaah hali ya kuwa ni wanyenyekevu.”
Pia imethibiti ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema kumwambia ´Imraan bin Huswayn (Radhiya Allaahu ´anh):
”Swali kwa kusimama. Usipoweza, kwa kukaa. Usipoweza, lalia bavu.”[2]
Vilevile imethibiti kutoka kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba alikuwa akiswali hali ya kusimama na akisema:
”Swalini kama mlivoniona nikiswali.”[3]
Yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwahi kuswali kwa kukaa isipokuwa katika hali ya kushindwa. Ni wajibu kwa wanaume na wanawake wote ambao wana jukumu juu ya matendo yao kuswali kwa kusimama – wakiweza kufanya hivo – katika swalah za faradhi. Hata hivyo hakuna neno kuswali kwa kukaa kwa sababu ya kushindwa kutokana na maradhi au utuuzima. Sijui kama kuna mwanachuoni yeyote ambaye ana mtazamo mwingine.
[1] 02:238
[2] al-Bukhaariy (1117).
[3] al-Bukhaariy (631).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ash-Sharh al-Mumtaaz, uk. 98
- Imechapishwa: 01/07/2018
Shaykh-ul-Islaam na Imaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Nguzo ya kwanza ni kusimama kwa mwenye kuweza. Dalili ni Kauli Yake (Ta ´ala):
حَافِظُوا عَلَى الصَّلَوَاتِ وَالصَّلَاةِ الْوُسْطَىٰ وَقُومُوا لِلَّـهِ قَانِتِينَ
”Zichungeni swalah na khaswa khaswa swalah ya katikati na simameni mbele ya Allaah hali ya kuwa ni wanyenyekevu.”[1]
MAELEZO
Kuhusiana na kusimama kwa mwenye kuweza, Allaah (Ta´ala) amesema:
وَقُومُوا لِلَّـهِ قَانِتِينَ
”… simameni mbele ya Allaah hali ya kuwa ni wanyenyekevu.”
Pia imethibiti ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema kumwambia ´Imraan bin Huswayn (Radhiya Allaahu ´anh):
”Swali kwa kusimama. Usipoweza, kwa kukaa. Usipoweza, lalia bavu.”[2]
Vilevile imethibiti kutoka kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba alikuwa akiswali hali ya kusimama na akisema:
”Swalini kama mlivoniona nikiswali.”[3]
Yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwahi kuswali kwa kukaa isipokuwa katika hali ya kushindwa. Ni wajibu kwa wanaume na wanawake wote ambao wana jukumu juu ya matendo yao kuswali kwa kusimama – wakiweza kufanya hivo – katika swalah za faradhi. Hata hivyo hakuna neno kuswali kwa kukaa kwa sababu ya kushindwa kutokana na maradhi au utuuzima. Sijui kama kuna mwanachuoni yeyote ambaye ana mtazamo mwingine.
[1] 02:238
[2] al-Bukhaariy (1117).
[3] al-Bukhaariy (631).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: ash-Sharh al-Mumtaaz, uk. 98
Imechapishwa: 01/07/2018
https://firqatunnajia.com/14-nguzo-ya-kwanza-ya-swalah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)