Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Dalili ya Qadar ni Kauli Yake (Ta´ala):
إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ
”Hakika kila kitu Sisi Tumekiumba kwa makadirio.”[1]
MAELEZO
Dalili ya nguzo ya sita katika nguzo za imani ni maneno Yake (Ta´ala):
إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ
”Hakika kila kitu Sisi tumekiumba kwa makadirio.”
Bi maana kila kilichoumbwa na Allaah kimekadiriwa katika elimu, uandishi na utashi Wake (Subhaanahu wa Ta´ala). Hakikutokea kiholela. Bali ni jambo limetangulia katika elimu ya Allaah, kimeandikwa katika ubao uliohifadhiwa na kimetangulia katika matakwa na utashi wa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).
[1] 54:49
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 221
- Imechapishwa: 26/01/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket