Swali: Je, inafaa kuwapa zakaah mizunguko ya kielimu inayosomesha Qur-aan?
Jibu: Hapana. Zakaah haitolewi kwa ajili ya kuhifadhi Qur-aan. Hawa wanapewa swadaqah na michango mingine. Wasipewi zakaah. Zakaah ni kwa ajili ya mafukara, masikini na aina nyenginezo zilizowekwa katika Shari´ah. Kuhusu nyanja zengine za mambo ya kheri wanapewa swadaqah na michango mingine. Miongoni mwa mataasisi hayo ni zile zinazojenga misikiti, masomo na kusomesha Qur-aan. Mataasisi kama haya hayapewi zakaah. Zakaah wanapewa wale watu aina saba.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (16)
- Imechapishwa: 23/04/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket