Zakaah juu ya ardhi ambayo mtu anasita kati ya kuiuza au kuifanya biashara

Swali: Kuna mtu yuko na ardhi na nia yake inasita na hajui aiuze, aijenge, aikodishe au ataishi juu yake. Je, aitolee zakaah baada ya kutimiza mwaka?

Jibu: Ardhi hii haitolewi zakaah muda wa kuwa hana uamuzi madhubuti juu ya kuifanyia biashara. Kwa hivyo hatoitolea zakaah maadamu ni mwenye mashaka. Hata angelikuwa na mashaka ya 1% basi asingeitolea zakaah.

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (18/232)
  • Imechapishwa: 17/05/2026