Yamini kwa mtu aliyeapa kutofanya kitu kwa hasira

Swali: Niliapa kuwa sintofanya kitu na nilikuwa na hasira sana. Lakini baada ya kujirudi nikafanya kitu kile. Je, juu yangu nina kafara ya yamini?

Jibu: Ikiwa hasira zilikupita kiasi cha kwamba huelewi unachokisema, huna yamini kwa kuwa hukuwa na malengo. Hichi ni kiapo cha upuuzi. Ama ikiwa unaelewa unachokisema na unakusudia kile unachokisema, juu yako una kafara.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (50) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1431-6-10.mp3
  • Imechapishwa: 21/08/2020