Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Kipenzi changu wa hali ya juu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliniusia mambo matatu: kufunga siku tatu za kila mwezi, Rak´ah mbili za dhuhaa na niswali Witr kabla ya kulala.”[1]
Wasia wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anapomzungumzisha mmoja katika Ummah wake basi ni kwamba amezungumzisha Ummah mzima muda wa kuwa hakuna dalili inayoonyesha kinyume chake.
Witr ni Sunnah iliyokokotezwa ambayo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliisisitiza na akadumu juu yake, ni mamoja katika hali ya ukazi na safarini.
Uchache wa swalah ya Witr ni Rak´ah moja. Mwenye kutaka anaweza pia kuswali Rak´ah tatu, tano, saba, tisa au Rak´ah kumi na moja. Anaweza kuziswali zote kwa Tasliym moja mwishoni au akatoa Tasliym kila baada ya Rak´ah mbili.
Witr inaanza kuanzia swalah ya ´Ishaa na inaenda mpaka kupambazuke alfajiri. Yule anayepangilia kuamka mwishoni mwa usiku bora aiswali wakati huo. Vinginevyo aiswali Witr mwanzoni mwame kama ilivyotajwa katika Hadiyth hii.
[1] al-Bukhaariy (1178), Muslim (721), at-Tirmidhiy (760), an-Nasaa’iy (1677), Abu Daawuud (1433) na Ahmad (7098, 7140 na 7409).
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdur-Rahmaan bin Naaswir as-Sa´diy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bahjat-ul-Abraar, uk. 85-87
- Imechapishwa: 03/03/2021
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Kipenzi changu wa hali ya juu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliniusia mambo matatu: kufunga siku tatu za kila mwezi, Rak´ah mbili za dhuhaa na niswali Witr kabla ya kulala.”[1]
Wasia wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anapomzungumzisha mmoja katika Ummah wake basi ni kwamba amezungumzisha Ummah mzima muda wa kuwa hakuna dalili inayoonyesha kinyume chake.
Witr ni Sunnah iliyokokotezwa ambayo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliisisitiza na akadumu juu yake, ni mamoja katika hali ya ukazi na safarini.
Uchache wa swalah ya Witr ni Rak´ah moja. Mwenye kutaka anaweza pia kuswali Rak´ah tatu, tano, saba, tisa au Rak´ah kumi na moja. Anaweza kuziswali zote kwa Tasliym moja mwishoni au akatoa Tasliym kila baada ya Rak´ah mbili.
Witr inaanza kuanzia swalah ya ´Ishaa na inaenda mpaka kupambazuke alfajiri. Yule anayepangilia kuamka mwishoni mwa usiku bora aiswali wakati huo. Vinginevyo aiswali Witr mwanzoni mwame kama ilivyotajwa katika Hadiyth hii.
[1] al-Bukhaariy (1178), Muslim (721), at-Tirmidhiy (760), an-Nasaa’iy (1677), Abu Daawuud (1433) na Ahmad (7098, 7140 na 7409).
Mhusika: ´Allaamah ´Abdur-Rahmaan bin Naaswir as-Sa´diy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Bahjat-ul-Abraar, uk. 85-87
Imechapishwa: 03/03/2021
https://firqatunnajia.com/witr-kila-siku-na-kila-mahali/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)