Waulize wanachuoni maswali kwa njia yoyote

Swali: Wakati ninapotatizwa na jambo niwaulize wanachuoni kwa njia ya simu au nitafute kwenye vitabu na tovuti za Fataawaa?

Jibu: Waulize wanachuoni kwa njia yoyote ile ambayo itakuwa ni nyepesi kwako…

Kuhusiana na kusikiliza kwenye mkanda na kuzifanyia kazi usifanye hivo. Kwa kuwa baadhi ya Fataawaa kwenye mikanda zinaweza kuwa za makosa na zingine wewe unaweza ukazifahamu kimakosa kinyume na makusudio ya mwanachuoni. Hakuna njia ya sawa isipokuwa kwa kuchukua Fatwa [moja kwa moja] kutoka kwa mwanachuoni ambaye umemuuliza. Usiichukue kwenye vitabu na kadhalika.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/adaab-11-08-1435-01.mp3
  • Imechapishwa: 01/05/2015