Swali: Watu wa Makkah kuhusu kupunguza swalah kwa ajili ya ´ibaadah?
Jibu: Wanafuata mahujaji, kwani Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwakubalia na hakuwakataza. Hakusema:
“Enyi watu wa Makkah, timizeni swalah.”
Kama alivyowaambia siku ya ufunguzi wa Makkah:
“Timizeni [swalah zenu], kwa kuwa sisi ni wasafiri.”
Swali: Ikiwa wako mbali na msikiti wa al-Namirah na hawawezi kusikia Khutbah?
Jibu: Wataswali wenyewe Dhuhr na ´Aswr kwa pamoja majumbani mwao.
Swali: Je, mmoja wao atawatolea Khutbah?
Jibu: Ikiwa mmoja wao atawakhutubia, basi hakuna tatizo. Na ikiwa watasikiliza kupitia vipaza sauti au redio, ni sawa.
Swali: Je, maneno ya baadhi ya wanazuoni kwamba kupunguza swalah kwa watu wa Makkah ni kwa sababu ya safari yana mashiko?
Jibu: Hapana, hayakupokelewa, kwa sababu baina ya Minaa na Makkah si umbali wa safari. Umbali wa Minaa na ´Arafah ni safari fupi.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25000/حكم-قصر-اهل-مكة-للصلاة-والنسك
- Imechapishwa: 22/01/2025
Swali: Watu wa Makkah kuhusu kupunguza swalah kwa ajili ya ´ibaadah?
Jibu: Wanafuata mahujaji, kwani Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwakubalia na hakuwakataza. Hakusema:
“Enyi watu wa Makkah, timizeni swalah.”
Kama alivyowaambia siku ya ufunguzi wa Makkah:
“Timizeni [swalah zenu], kwa kuwa sisi ni wasafiri.”
Swali: Ikiwa wako mbali na msikiti wa al-Namirah na hawawezi kusikia Khutbah?
Jibu: Wataswali wenyewe Dhuhr na ´Aswr kwa pamoja majumbani mwao.
Swali: Je, mmoja wao atawatolea Khutbah?
Jibu: Ikiwa mmoja wao atawakhutubia, basi hakuna tatizo. Na ikiwa watasikiliza kupitia vipaza sauti au redio, ni sawa.
Swali: Je, maneno ya baadhi ya wanazuoni kwamba kupunguza swalah kwa watu wa Makkah ni kwa sababu ya safari yana mashiko?
Jibu: Hapana, hayakupokelewa, kwa sababu baina ya Minaa na Makkah si umbali wa safari. Umbali wa Minaa na ´Arafah ni safari fupi.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25000/حكم-قصر-اهل-مكة-للصلاة-والنسك
Imechapishwa: 22/01/2025
https://firqatunnajia.com/watu-wa-makkah-kupunguza-swalah/