Swali: Mimi ni mwalimu wa Qur-aan. Je, wanafunzi wanawajibika kutawadha kabla ya kugusa msahafu au katika kipindi cha Qur-aan?

Jibu: Ndiyo, wanafunzi wanapaswa kutawadha ili kugusa msahafu. Haya ndio maoni ya kikosi kikubwa cha wanazuoni, wakiwemo maimamu wanne na wengineo. Imekuja katika Hadiyth ya ´Amr bin Hazm kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwaandikia watu wa Yemen:

“Asiiguse Qur-aan isipokuwa aliye twahara.”

Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) walitoa fatwa kwa hilo na wakaamrisha kutawadha kwa ajili ya kugusa Qur-aan. Kwa hiyo ikiwa wanafunzi wanataka kugusa msahafu ni lazima watawadhe.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/3229/حكم-مس-المصحف-بدون-وضوء
  • Imechapishwa: 02/08/2026