Swali: Dada huyu anauliza ni ipi hukumu ya wanafunzi wa kike kuremba sauti zao wakati wa kusoma Qur-aan mbele ya mwalimu wa kiume katika chuo kikuu pamoja na kuwa mwanamke hakutakiwa kufanya hivo?
Jibu: Sionelei apambe sauti yake. Kwa sababu Allaah (Ta´ala) amesema:
فَلَا تَخْضَعْنَ بِالْقَوْلِ فَيَطْمَعَ الَّذِي فِي قَلْبِهِ مَرَضٌ وَقُلْنَ قَوْلًا مَّعْرُوفًا
“Hivyo basi msilegeze kauli asije akaingiwa tamaa ambaye moyoni mwake mna maradhi na semeni kauli inayokubalika.”[1]
Kule mwanafunzi wa kike kusoma Qur-aan kwa utaratibu ipasavyo na utungo na kwa kuremba sauti kunakhofiwa fitina. Inatosha kwake kusoma Qur-aan kisomo cha kawaida.
[1] 33:32
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (42) http://binothaimeen.net/content/927
- Imechapishwa: 04/12/2018
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket