Wanaume wengi wamefitinishwa na wanawake kwa mbinu hii

Swali: Je, inajuzu kumwangalia mwanamke mwenye kuonyesha mapambo yake ambaye anakuwa katika baadhi ya chaneli katika taarifa ya khabari pasi na moyo wa mtazamaji kumili kwake?

Jibu: Asikilize taarifa ya khabari pasi na kumwangalia mwanamke. Aangalie taarifa ya khabari inayotolewa na mwanaume. Vinginevyo asikilize redioni. Asimwangalie mwanamke. Mwanamke ni fitina vovyote iwavyo. Wamewafitinisha waislamu kwa njia hii. Ni wajibu kwa muislamu ajikinge na kujitenga mbali na mambo haya.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (62) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1432-03-18.MP3
  • Imechapishwa: 21/08/2020