Abul-Waliyd al-Faqiyh amesema: “Nilimsikia Ibn Rurayj akisema:
“Ni mara chache nimemuona msomi anayejishughulisha na falsafa akafaulu. Isitoshe atapitwa na elimu na hatofikia falsafa yenyewe.”
al-Haakim amesema: Nimemsikia Hassaan bin Muhammad akisema:
“Mwaka 303 tulikuwa katika kikao cha elimu cha Ibn Surayj ambapo akasimama mwanachuoni mmoja na kusema: “Pata bishara njema, ee hakimu! Kwani Allaah hutuma kila baada ya miaka mia mtu ambaye anaihuisha dini Yake.” Karne ya kwanza Allaah alimtuma ´Umar bin ´Abdil-´Aziyz, karne ya pili akamtuma Muhammad bin Idriys ash-Shaafi´iy na karne ya tatu akakutuma wewe.”
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (14/202-203)
- Imechapishwa: 09/11/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)