Swali: Jopo la watu wamesahau kuswali ´Aswr na hawakukumbuka isipokuwa wakati waliposikia kunaadhiniwa Maghrib. Wakaanza kuswali Maghrib kisha baadaye ´Aswr. Ni ipi hukumu?
Jibu: Mtu akisahau swalah au usingizi ukamchukua na asiwe na mtu wa kumuamsha au kumkumbusha mpaka ukatoka wakati wake, mambo ni kama alivosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yule mwenye kupitikiwa na usingizi au akaisahau swalah, basi aiswali pale atapoikumbuka. Haina kafara nyingine isipokuwa hiyo.”[1]
Katika hali kama hii ya muulizaji anatakiwa kwanza kuswali ´Aswr kisha Maghrib, ili mpangilio iwe vile alivyofaradhisha Allaah (´Azza wa Jall). Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipopitwa na swalah kadhaa katika vita vya Khandaq alizilipa kwa mpangilio. Vilevile Mtume (Swalla Allaahu ´alayi wa sallam) amesema:
“Swalini kama mlivyoniona nikiswali.”[2]
Wakati mlipokuja msikitini na mkawakuta watu wanaswali Maghrib, mngejiunga nao kwa nia ya ´Aswr. Kisha wakati imamu atakapomaliza kuswali Maghrib, mkakamilisha swalah yenu la ´Aswr. Hivyo mkawa mmeswali Maghrib kwa mkusanyiko na ´Aswr kivyenu. Kutofautiana kwa nia ya imamu na maamuma haidhuru. Kwa sababu matendo ni yaleyale. Alichokataza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni kutofautiana na imamu kimatendo na si kinia. Kwa mle mlifanya kwa ujinga ambapo mlianza kuswali Maghrib kabla ya ´Aswr, haina neno juu ya jambo hilo.
[1] al-Bukhaariy (597) na Muslim (684).
[2] al-Bukhaariy (631).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/223)
- Imechapishwa: 15/04/2026
Swali: Jopo la watu wamesahau kuswali ´Aswr na hawakukumbuka isipokuwa wakati waliposikia kunaadhiniwa Maghrib. Wakaanza kuswali Maghrib kisha baadaye ´Aswr. Ni ipi hukumu?
Jibu: Mtu akisahau swalah au usingizi ukamchukua na asiwe na mtu wa kumuamsha au kumkumbusha mpaka ukatoka wakati wake, mambo ni kama alivosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yule mwenye kupitikiwa na usingizi au akaisahau swalah, basi aiswali pale atapoikumbuka. Haina kafara nyingine isipokuwa hiyo.”[1]
Katika hali kama hii ya muulizaji anatakiwa kwanza kuswali ´Aswr kisha Maghrib, ili mpangilio iwe vile alivyofaradhisha Allaah (´Azza wa Jall). Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipopitwa na swalah kadhaa katika vita vya Khandaq alizilipa kwa mpangilio. Vilevile Mtume (Swalla Allaahu ´alayi wa sallam) amesema:
“Swalini kama mlivyoniona nikiswali.”[2]
Wakati mlipokuja msikitini na mkawakuta watu wanaswali Maghrib, mngejiunga nao kwa nia ya ´Aswr. Kisha wakati imamu atakapomaliza kuswali Maghrib, mkakamilisha swalah yenu la ´Aswr. Hivyo mkawa mmeswali Maghrib kwa mkusanyiko na ´Aswr kivyenu. Kutofautiana kwa nia ya imamu na maamuma haidhuru. Kwa sababu matendo ni yaleyale. Alichokataza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni kutofautiana na imamu kimatendo na si kinia. Kwa mle mlifanya kwa ujinga ambapo mlianza kuswali Maghrib kabla ya ´Aswr, haina neno juu ya jambo hilo.
[1] al-Bukhaariy (597) na Muslim (684).
[2] al-Bukhaariy (631).
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/223)
Imechapishwa: 15/04/2026
https://firqatunnajia.com/wameswali-maghrib-kabla-ya-aswr-kwa-kusahau/