Ni haramu kuichelewesha swalah mpaka ukatoka wakati wake

Swali: Nini afanye ambaye anafanya hajj akichelewa kutoka ´Arafah kutokana na msongamano mkubwa na akakhofia kutoka wakati wa ´Ishaa kabla ya kufika Muzdalifah?

Jibu: Akikhofia kutoka kwa wakati, basi atalazimika kushuka na kuswali. Baadhi ya mahujaji hawaswali Maghrib na ´Ishaa mpaka wafike Muzdalifah ijapo umekwishatoka wakati wa swalah ya ´Ishaa. Kitendo hicho hakijuzu. Ni haramu na ni dhambi kubwa. Kwa mujibu wa dalili ya Qur-aan na Sunnah ni haramu kuchelewesha swalah mpaka ukatoka wakati wake. Allaah (Ta´ala) amesema:

إِنَّ الصَّلَاةَ كَانَتْ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ كِتَابًا مَّوْقُوتًا

“Kwani hakika swalah kwa waumini ni fardhi iliyowekwa nyakati maalum.”[1]

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amebainisha na kuzipanga nyakati hizi. Allaah (Ta´ala) amesema:

وَتِلْكَ حُدُودُ اللَّـهِ ۚ وَمَن يَتَعَدَّ حُدُودَ اللَّـهِ فَقَدْ ظَلَمَ نَفْسَهُ

”Hiyo ndio mipaka ya Allaah; na yeyote atakayevuka mipaka ya Allaah, basi kwa hakika ameidhulumu nafsi yake.”[2]

تِلْكَ حُدُودُ اللَّـهِ فَلَا تَعْتَدُوهَا ۚ وَمَن يَتَعَدَّ حُدُودَ اللَّـهِ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ

”Hiyo ni mipaka ya Allaah, hivyo basi msivuke mipaka; yeyote atakayevuka mipaka ya Allaah basi hao ndio madhalimu.”[3]

[1] 04:103

[2] 65:1

[3] 2:229

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/205-206)
  • Imechapishwa: 15/04/2026