Swali: Nini maana ya kwamba tawbah inakubaliwa muda wa kuwa mtu hajasagasaga miguu?
Jibu: Maana yake ni kwamba muda wa kuwa haujafika muda wa kukata roho baada ya kumuona Malaika wa kifo.
Swali: Vipi kuhusu maneno yake Fir´awn:
حَتَّىٰ إِذَا أَدْرَكَهُ الْغَرَقُ قَالَ آمَنتُ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا الَّذِي آمَنَتْ بِهِ بَنُو إِسْرَائِيلَ وَأَنَا مِنَ الْمُسْلِمِينَ
”… mpaka ilipomfikia kuzama akasema: ”Nimeamini kwamba hapana mungu wa haki, isipokuwa Yule waliyemwamini wana wa israaiyl, na mimi ni miongoni mwa waislamu.”[1]?
Jibu: Imani yake hii haikumfaa kitu kwa sababu adhabu imeshashuka. Amesema (Ta´ala):
فَلَمَّا رَأَوْا بَأْسَنَا قَالُوا آمَنَّا بِاللَّـهِ وَحْدَهُ وَكَفَرْنَا بِمَا كُنَّا بِهِ مُشْرِكِينَ فَلَمْ يَكُ يَنفَعُهُمْ إِيمَانُهُمْ لَمَّا رَأَوْا بَأْسَنَا
”Walipoiona adhabu Yetu walisema: ”Tumemuamini Allaah pekee na tunayakanusha vile ambavyo tulikuwa tunamshirikisha Naye. Haikuwa imani yao ni yenye kuwafaa pale walipoona adhabu Yetu.”[2]
Adhabu inaposhuka tawbah hainufaishi. Wakati kina Thaamuud na kina ´Aad walipoteremkiwa na adhabu tawbah haikuwanufaisha kitu. Tawbah inakubaliwa kabla ya hapo.
[1] 10:90
[2] 40:84-85
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24572/معنى-تقبل-التوبة-ما-لم-يغرغر
- Imechapishwa: 04/11/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket